Kituo cha kulelea watoto yatima na wenye mahitaji maalum cha Chipole, kilichopo Kata ya Magagura, Halmashauri ya Songea Vijijini mkoani Ruvuma, kimepokea msaada wa fedha taslimu shilingi milioni 1.2, vyakula, nguo na mahitaji mengine muhimu kutoka Jumuiya ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) ikihusisha wafanyakazi, wanafunzi, wahitimu na wadau mbalimbali.
Akikabidhi msaada huo, Mhadhiri Msaidizi Vincent Mpepo alisema chuo kimeguswa na changamoto za watoto hao na kuahidi kushirikiana na uongozi wa OUT kufadhili bima za afya kwa watoto 50 ili kusaidia upatikanaji wa matibabu.
Kwa upande wake, Inspekta Dominic Msangi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma alisema msaada huo ni sehemu ya mkakati wa Kamishna wa Polisi Jamii wa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kusaidia makundi maalum.
Akizungumza kwa niaba ya kituo, hicho Mtawa Maria Akwinata O.S.B aliishukuru OUT na Jeshi la Polisi kwa msaada huo, akibainisha kuwa kulea watoto hao kunahitaji msaada endelevu.
Watoto kupitia mwakilishi wao, Richard Haule, waliwashukuru wadau hao na kuomba jamii kuendelea kujitokeza kuwasaidia kwa ajili ya maisha yao ya baadaye.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.