Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania (CGI) Dkt. Anna Makakala amefanya ziara ya pamoja ya kikazi na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji nchini (IOM) Bw. Maurizio Busatti kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi katika Kituo cha Uhamiaji Mpaka wa Mkenda–Nakawale wilayani Songea mkoani Ruvuma.Mradi huo unaofadhiliwa na IOM unalenga kuboresha mazingira ya kazi na kuhakikisha watumishi wa Idara ya Uhamiaji wanapata makazi bora, salama na yanayokidhi viwango vya kimataifa, hatua itakayoongeza ufanisi na motisha kazini.Dkt. Makakala ameridhishwa na kasi na ubora wa utekelezaji wa mradi huo, akieleza kuwa unatekelezwa kwa viwango vinavyokubalika kitaalamu, huku akiishukuru IOM kwa kuendeleza ushirikiano thabiti na Serikali ya Tanzania.Kwa upande wake, Bw. Busatti amesema ujenzi unazingatia michoro na viwango vilivyobainishwa, na kusisitiza kuwa IOM itaendelea kushirikiana na Idara ya Uhamiaji katika miradi mingine ya maendeleo.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.