Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, amefungua rasmi maktaba ya mkoa wa Ruvuma iliyopo katika Manispaa ya Songea baada ya kukamilika kwa ukarabati wake uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 134.
Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Brig. Jen. Ahmed Abbas amewataka wanafunzi, walimu na jamii kwa ujumla kuitumia maktaba hiyo kama daraja la kufikia mafanikio, akiwasisitiza vijana kuitumia kukuza ubunifu, kufanya tafiti na kuibua mawazo mapya yatakayowanufaisha wao binafsi na taifa kwa ujumla.
Amesema ukarabati wa maktaba hiyo ni hatua kubwa ya kimaendeleo inayogusa kizazi cha sasa na kijacho. Kupitia Bodi ya Huduma za Maktaba, serikali imeongeza miundombinu ya kisasa ikiwemo teknolojia ya Tehama, ili kuhakikisha jamii inapunguza pengo la maarifa na kuendana na mabadiliko ya dunia ya sasa.
Vilevile mebainisha kuwa maktaba hiyo itasaidia kuongeza usawa wa fursa, kujenga uchumi wa kisasa wa viwanda na kuimarisha matumizi ya Tehama.
Brig. Jen. Ahmed Abbas amesisitiza kuwa ni wajibu wa jamii nzima ikiwemo serikali na wadau mbalimbali kuitunza na kuitumia kikamilifu maktaba hiyo kwa kuwa ni mikakati ya serikali kuhakikisha kila Mtanzania anapata nafasi ya kusoma, kufanya utafiti, kujifunza teknolojia mpya na kutumia taarifa sahihi kwa maendeleo binafsi na ya taifa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Huduma za Maktaba Nchini, Dkt. Mboni Ruzegea, amesema wana imani kubwa kuwa baada ya kukamilika kwa ukarabati na kufunguliwa upya, idadi ya watumiaji itaongezeka maradufu, kwani maktaba hiyo sasa imeboreshwa na ina miundombinu ya kisasa inayokidhi mahitaji ya jamii
Maktaba hiyo ya mkoa wa Ruvuma ilianzishwa rasmi Juni 30, 1990 ikiwa ni sehemu ya mkakati wa serikali kuhakikisha kila mkoa unakuwa na kituo cha kujisomea na kuongeza maarifa.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.