Katika nyakati ambazo dunia inashuhudia changamoto za kiafya zinazobadilika kwa kasi, Mkoa wa Ruvuma umeibuka kama mfano wa utekelezaji bora na wa matokeo katika kuboresha huduma za afya.
Ni mageuzi ambayo hayajaanza tu kuonekana kwenye takwimu, bali kwenye uso wa kila mwananchi anayepata huduma kwa wakati, usalama na heshima. Ndiyo maana Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, anasema kwa uthabiti kuwa “mkoa umedhamiria kuboresha sekta ya afya kwa vitendo, ili wananchi wapate huduma bora na stahiki bila vikwazo.”
Hii ni simulizi ya safari ya mageuzi katika sekta ya afya yenye takwimu zinazozungumza, sera zinazoongoza hatua, na matokeo yanayoonekana kwa macho.
Mtandao wa Vituo 494: Uhai Unaogusa Kila Kijiji
Ruvuma ina mtandao mpana wa vituo 494 vya afya unaounda uti wa mgongo wa huduma zake. Hospitali 18 kati ya hizo tisa za Serikali, saba za Mashirika ya Dini na mbili za binafsindizo nguzo kuu,zinaungwa mkono na vituo vya afya 57 na zahanati 364 ambazo zinawafikia wananchi hadi maeneo ya pembezoni.
Mtandao huu umekuwa na thamani zaidi kutokana na hatua kubwa katika upatikanaji wa dawa. Leo hii hali imeimarika na kufikia upatikanaji wa dawa kwa asilimia 87. Mkoani Ruvuma, msongamano, safari ndefu za kutafuta dawa na kusubiri kwa muda mrefu, ni simulizi zinazofifia taratibu.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.