Mwambao wa Ziwa Nyasa mkoani Ruvuma imeandikwa historia ya dunia kabla wengi hawajazaliwa. Agosti 1914, Bandari ya Liuli, ikijulikana zaidi kwa Hospitali ya Mtakatifu Anna inayomilikiwa na kanisa Anglikana Dayosisi ya Ruvuma ikawa eneo la ushindi wa kwanza wa Waingereza wa majini katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia barani Afrika.
Hapa ndipo Waingereza walipoizima na baadaye kuizamisha **Hermann von Wissmann**, meli pekee ya kivita ya Wajerumani katika Ziwa Nyasa. Meli hiyo yenye urefu wa mita 60 yenye mzinga na uwezo wa kubeba askari 150, ilikuwa ishara ya udhibiti wa Ujerumani ziwani na tishio kwa maslahi ya Uingereza.
Kinachofanya simulizi hii kuwa ya kipekee ni kwamba makamanda wa pande hasimu,Nahodha Mwingereza Edmund Rhoades na Nahodha Mjerumani Berndt,walikuwa marafiki kabla ya vita. Lakini amri ya kijeshi ilibadilisha urafiki kuwa mapambano. Kwa kutumia mzinga uliowekwa ufukweni, Waingereza waliiharibu meli hiyo karibu na Liuli, ushindi uliotangazwa London Uingereza kama *“Naval Victory on Lake Nyasa.”*
Leo, maboya yanayoelea Liuli yanaashiria mahali meli ilipozama,urithi adimu wa vita ya majini iliyopiganwa ziwani, si baharini. Historia hii bado inasubiri kusimuliwa dunia nzima.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.