• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

FAHAMU uhusiano uliopo kati ya Pori la Akiba Liparamba na ziwa Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: October 26th, 2021

Ni mbuga chache za wanyama pori hapa nchini ambazo zimebahatika kuwa na maingilio au mapitio ya wanyama ambayo yanaitwa ushoroba kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine jirani .

Pori la wanyamapori Liparamba lililopo wilayani  Nyasa mkoani Ruvuma ni miongoni mwa mapori yaliyopitiwa na ushoroba wa wanyama.

Afisa Utalii wa Pori hilo Maajabu Mbogo amesema pori hilo ambalo lilianzishwa mwaka 2000,limebahatika kuwa na wanyamapori wakubwa na wadogo wakiwemo tembo,simba, chuo,viboko,mamba,tandala,pofu,palahala,kuro,nyati, pundamilia,fisi,chui na mbweha na  ndege kama vile kanga, koribustard(Mbawala) na fundichuma.

“Neno liparamba ni la kabila la kimatengo ambao ni wenyeji wanaoishi wilaya ya Mbinga,maana liparamba ni mbuzimawe,pori hili lina makundi makubwa ya tembo,ambao ni wakimbizi kwa sababu huwa wanatoka Msumbiji na kuhamia Liparamba’’,alisema Mbogo.

Amesema makundi makubwa ya tembo kutoka Msumbiji yanaingia kwa wingi katika pori la Liparamba kuanzia mwezi Machi kila mwaka na kufikia mwezi Julai,tembo wanaanza kurudi nchini Msumbiji na kwamba inapofika kati ya Septemba na Oktoba wanabaki tembo wachache sana ndani ya hifadhi hiyo.

“Inapotokea kule nchini Msumbiji majangili yamewashambulia tembo au kuwasumbua,tembo hao wanapoingia katika hifadhi ya Liparamba hawatoki,wanabaki ndani ya pori la Liparamba kati ya miaka miwili hadi mitatu bila kutoka na kurudi Msumbiji kwa sababu Liparamba ni sehemu salama ya kuishi tembo’’,alisisitiza.

Amesema katika pori la Liparamba pia amewahi kuonekana simba mweupe na kwamba jambo hilo sio kitu cha ajabu  kwa kuwa viumbe hai wakiwemo wanyama na mimea ikipata kasoro kwenye ngozi au majani inaweza kuwa na rangi nyeupe.

Anavitaja vivutio vingine vilivyopo katika pori hilo ni uwepo wa aina mbalimbali za  nyoka kama vile jamii ya mamba na kobra na kwamba pori hilo limepitiwa na mito 25 yakiwemo  maporomoko ya  maji ya Nakatuta katika Mto Ruvuma ambayo ni kivutio cha asili cha utalii.

Kwa mujibu wa Afisa Utalii huyo,pori hilo lina vivutio vinavyofaa kufanya utalii wa kupanda kwenye mawe kwa sababu ndani ya hifadhi hiyo,kuna mawe makubwa yanayofaa kwa utalii wa aina hiyo.

Amesema ndani ya pori hilo kuna miti ya ajabu ukiwemo mti wa mtetereka ambao ukikauka unabadilika na kuwa jiwe na kwamba miti ya aina hiyo ipo kwa wingi katika eneo la Nakatuta kandokando mwa Mto Ruvuma hivyo kuvutia watalii wengi wanaopenda kufanya utafiti wa miti na mimea.

Katika eneo la Mkuyu ndani ya pori la Liparamba pia kuna kivutio kinachowashangaza wengi ambacho,maji yanayotiririka kwenye mto Mkuyu yametengeneza mfano wa ramani ya Afrika juu ya mwamba.

“Maji yameweza kutengeneza mfano wa ramani ya Afrika juu ya mwamba,ukichukua ramani ya Afrika na kuangalia ramani iliyotengenezwa na maji hakuna tofauti ni ramani kabisa ya Afrika,haya ni moja ya maajabu katika pori la Liparamba’’,alisema Mbogo.

Kwa upande wake Mhifadhi Msaidizi wa pori hilo Paul Protas  anakitaja kivutio kingine kilichopo katika pori hilo ni uwepo wa ndege aina ya koribustard(Mbawala) ambaye hapa nchini anatumika kama alama ya Taifa kama ilivyo kwa mnayama twiga.

“Huyu ni ndege mkubwa  ana uwezo wa kufikisha uzito KG 16,ana urefu wa SM 1330,huyu ni ndege wa kitaifa,anachinjwa  kwa kibali kinachoombwa kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania’’,anasisitiza.

Pori la akiba Liparamba lina muunganiko wa moja kwa moja na ziwa Nyasa hivyo mtalii akimaliza kuangalia vivutio vya utalii ndani ya pori la Akiba Liparamba anaendelea na utalii kupitia milima ya Livingistone ambayo imeshuka moja kwa moja kwende Bonde la ufa hadi ziwa Nyasa.

Afisa Utalii wa Pori la Akiba Liparamba Maajabu Mbogo anasema ukitoka Liparamba unashuka na milima ya Livingstone ambayo ni maarufu duniani ma kukutana na ziwa Nyasa lenye vivutio lukuki vya utalii.

“Hili ni ziwa adimu duniani,ni benki ya vivutio vya utalii,lina aina zaidi ya 400 za samaki wa mapambo,lina fukwe za asili za kuvutia,visiwa vya kuvutia,eneo la ziwa Nyasa ndiyo eneo pekee duniani ambalo mabonde mawili ya ufa la mashariki na Magharibi yamekutana’’alisema Mbogo.

Hata hivyo amesema maeneo ya milima ya Livingstone kando mwa ziwa Nyasa ndiyo ,maeneo ambayo ndege wahamiaji toka bara la Ulaya na maeneo mengine duniani wanapumzika kabla ya kuendelea na safari.

Utafiti umebaini kuwa Liparamba ni  eneo  kipekee duniani lililopo katika ukanda wa juu wa misitu ya miombo lenye msitu mnene wa asili na wenye mandhari ya kuvutia . 

Makala imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 26.2021

         

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.