Hatimaye ndoto ya kuunganisha Wilaya ya Nyasa na Songea mkoani Ruvuma inakaribia kutimia!
Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS Ruvuma imeanza ujenzi wa daraja la kisasa la Mitomoni lenye urefu wa mita 45 kwenye Mto Ruvuma.
Gharama ya Mradi ni shilingi Bilioni 9.295 (Fedha za Benki ya Dunia)
Mkandarasi: Ovans Construction Ltd
Hali ya Mradi: Umefikia 65%
Utarajiwa Kukamilika: Septemba 2025
Daraja hili litaunganisha barabara za Unyoni–Mpapa–Lipalamba–Mkenda na Likuyufusi–Mkenda, na litakuwa na:
✅ Njia mbili za magari
✅ Njia za watembea kwa miguu pande zote mbili
✅ Barabara unganishi ya lami ya km 8
Meneja wa TANROADS Ruvuma, Mhandisi Saleh Juma, amesema daraja hili litakuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi, likitatua kero ya kukwama upande mmoja wa mto wakati wa masika. Pia litaimarisha:
Mawasiliano kati ya Nyasa, Songea na Msumbiji
Biashara na usafirishaji wa bidhaa
Upatikanaji wa huduma za kijamii
Maendeleo ya uchumi wa Mkoa
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.