• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UMUHIMU wa mtoto kunyonya maziwa ya Mama

Imewekwa kuanzia tarehe: August 7th, 2023

Watoto wachanga wanapaswa kuanza kunyonyeshwa maziwa ya mama ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa ili maziwa yaanze kutoka mapema.

Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) wanaeleza kuwa inashauriwa mara baada ya kujifungua mama na mtoto wagusane ngozi kwa ngozi ili kusaidia maziwa kutoka na kuongeza uhusiano kati ya mama na mtoto. Ni muhimu kwa mtoto kuwekwa kwenye titi ili aanze kunyonya maziwa ya mama.

Mama na mtoto wasitenganishwe, wawe pamoja muda wote, ila wanaweza kutenganishwa kwa ushauri wa daktari ikiwa kuna tatizo litakalomuathiri mtoto akiwa na mama yake mfano ugonjwa wa mtoto au mama.

Kumnyonyesha mtoto ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa kuna faida nyingi ikiwemo:

  • Kusaidia maziwa ya mama kuanza kutoka mapema na mtoto kupata maziwa ya mwanzo ya njano.
  • Kusaidia tumbo la uzazi kurudi katika hali yake ya awali na kupunguza kutoka damu nyingi baada ya kujifungua.
  • Kusaidia kumpa mtoto joto
  • Kujenga uhusiano wa kihisia na upendo kati ya mama na mtoto
  • Kusaidia kuchochea maziwa kutoka kwa wingi

Umuhimu wa maziwa ya njano kwa mtoto

Maziwa ya njano ni maziwa ya mwanzo, mazito yenye rangi ya njano ambayo hutoka siku chache za mwanzo baada ya kujifungua. Maziwa haya ni chakula kamili chenye virutubishi vingi, na pia yanatoa kinga maalum dhidi ya maradhi.

Aidha maziwa ya njano humsaidia mtoto kutoa kinyesi cha mwanzo chenye rangi ya kijani au nyeusi ambacho humfanya mtoto aumwe tumbo siku za mwanzo kama hatanyonya.

Virutubisho vilivyomo kwenye maziwa ya mama

Maji 87%

Wanga 7%

Mafuta 4%

Protin 1%

Vingine 1% (Vitamini, madini, kingamwili, vimeng'enya, Kiinitete)

Kunyonyesha kunampunguza hatari ya magonjwa kwa mtoto, mama

Mtoto anaponyonya inaweza kumsaidia kupunguza hatari ya kupata magonjwa yafuatayo:

Pumu

Unene kupita kiasi

Aina 1 ya kisukari

Ugonjwa mkali wa kupumua kwa chini

Maambukizi ya sikio

Ugonjwa wa kifo cha ghafla cha watoto wachanga (SIDS)

Maambukizi ya njia ya utumbo

Mama anaponyonyesha inaweza kupunguza hatari ya kupata magonjwa yafuatayo:

Shinikizo la damu

Aina ya 2 ya kisukari

Saratani ya ovari

Saratani ya matiti

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.