• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUHILA Zoo,almasi ya utalii inayong'aa katikati ya mji wa Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: July 20th, 2025

Ni umbali wa kilometa nane tu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, lakini Bustani ya Ruhila ni safari ya kipekee kuelekea kwenye utulivu, asili na mandhari ya kupendeza isiyo na mfano. Hii si bustani ya kawaida—ni hazina ya utalii wa wanyamapori inayokua kwa kasi chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Kanda ya Kusini Mashariki.

Asili ya Ruhila inarutubishwa na historia ya zaidi ya nusu karne ya uhifadhi. Tangu mwaka 1973 hadi sasa, eneo hili limepitia mikononi mwa mamlaka mbalimbali hadi kufikia usimamizi wa TAWA mwaka 2017, hatua iliyofungua ukurasa mpya wa uwekezaji wa kisasa katika sekta ya utalii mkoani Ruvuma.

 Wanyama, Uoto na Hadithi ya Ruhila

Ofisa Mhifadhi wa TAWA, Daudi Tesha, anasimulia kuwa jina "Ruhila" lilitokana na mto wenye maporomoko ya kihistoria uliowahi kusababisha watu wengi “kuhira” au kuzama — hatimaye likazaliwa jina Ruhila. Mto huo unapita katikati ya bustani, ukiupa uzuri wa asili unaovutia.

Ndani ya Ruhila Zoo kuna aina mbalimbali za wanyama walioachwa huru wakiwemo pundamilia, nyumbu, pofu, swala pala, digidigi na kuro. Aidha, wanyama wakali kama simba, chui na tembo wamewekwa kwenye vizuizi maalum, hali inayowezesha wageni kuwaona kwa usalama.

Bustani imezungukwa na uoto wa asili wa miti ya miyombo, misukusuku na mipangapanga ambayo imehifadhiwa kwa zaidi ya miaka 50 bila kuharibiwa. Mazingira haya yanaiweka Ruhila kuwa bustani pekee ya mji yenye uzuri wa pori la kweli.

 Vivutio vya Kiutalii na Fursa za Uwekezaji

Ruhila si sehemu ya kuangalia tu wanyama. Imeboreshwa kwa huduma zinazowafanya wageni kuifurahia bustani hiyo kwa njia nyingi zaidi. Vibanda vya kupumzika, bwawa la kuogelea, michezo ya watoto, baskeli na magari madogo yanayozunguka bustani yote ni sehemu ya burudani zinazopatikana.

Aidha, eneo maalum la kupiga kambi lina miundombinu ya maji, umeme na mawasiliano—likiwa salama na rafiki kwa watalii. Kiingilio ni cha kawaida: Sh 5,900 kwa watoto na Sh 11,800 kwa watu wazima.

Fursa za uwekezaji ni nyingi. Kutoka kwa hoteli, huduma za chakula na vinywaji, hadi uwekezaji wa kambi za mahema kando ya Mto Ruhila. Hata miundombinu ya utalii wa kutembea kwa kutumia vitoroli vya waya imepangwa kuanzishwa kutokana na bonde na miti mikubwa inayozunguka eneo hilo.

 Ruhila Katika Ramani ya Dunia

Kwa mujibu wa Tesha, TAWA ina mpango wa kuongeza idadi ya wanyama wa kupendezesha zaidi bustani, akiwemo twiga, mbuni na swala wanaoweza kuingiliana kwa karibu na watalii—ikiwemo kupigwa nao picha na kuwalisha.

Aidha, vizimba vya kutembea vinavyobeba wanyama vinaandaliwa kwa ajili ya kuwafikia watu wasio na muda wa kuitembelea bustani moja kwa moja.

Lakini zaidi ya yote, ni mshikamano wa jamii ya Songea unaoifanya Ruhila kuwa kivutio salama na endelevu. “Wananchi wamekuwa walinzi wakuu wa rasilimali hii. Tunawashukuru kwa moyo wa uzalendo wa kweli,” anasema Tesha.

  Ruhila Zoo, Ndoto Inayokuja Kuwa Alama ya Utalii wa Kusini

Kwa mipango na uwekezaji unaofanyika, Ruhila Zoo iko mbioni kuwa kivutio kikuu cha Afrika Mashariki. Ndoto ya Tesha ni kuiona Ruhila ikitajwa Kigali, Kampala, Nairobi, hata Paris. Ni ndoto inayowezekana ikiwa juhudi za serikali, wawekezaji, na jamii zitaungana kwa pamoja.

Ruhila si tu bustani—ni urithi hai wa Songea unaohitaji kuenziwa, kutembelewa na kuwekewa nguvu mpya kila siku. Karibu Ruhila, penye pumzi ya asili, sauti za wanyama, na ahadi ya uzuri usioisha.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RUHILA Zoo,almasi ya utalii inayong'aa katikati ya mji wa Songea

    July 20, 2025
  • LANGO la Namtumbo,mlango mpya wa utalii unaofungua uchumi wa Ruvuma

    July 18, 2025
  • MISITU ya vijiji inavyoibadilisha Ruvuma kuwa ngome ya kijani ya uchumi mpya

    July 16, 2025
  • DC NAMTUMBO awapongeza mashujaa wa uhifadhi

    July 16, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.