• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA yaandika historia chupa 4040 za damu zakusanywa kuokoa maisha

Imewekwa kuanzia tarehe: June 15th, 2025

Mkoa wa Ruvuma umeandika historia mpya baada ya kuadhimisha Siku ya Uchangiaji Damu Duniani kwa mafanikio makubwa, huku viongozi wa serikali, taasisi na wananchi wakijitokeza kwa wingi kuunga mkono zoezi hilo la kuokoa maisha.

Akihutubia umati wa wananchi katika viwanja vya Manispaa ya Songea, Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo, Michael Mbano, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, alisema kaulimbiu ya mwaka huu  “Changia damu, leta matumaini — pamoja tunaokoa maisha”  inabeba wito wa umoja na mshikamano wa jamii.

Mbano alisema  kuwa, kuanzia Januari hadi Juni 12, 2025, mkoa umekusanya chupa 4,040 za damu, ikiwa ni asilimia 27 ya lengo la mwaka mzima. Alibainisha kuwa mafanikio haya yamekuja kutokana na hamasa ya wananchi, taasisi, na dini, waliojitokeza kuchangia bila kusita.

Akielezea mikakati ya serikali, Mbano alisema huduma za afya zinaimarika siku hadi siku, kupitia uboreshaji wa majengo, upatikanaji wa vifaa tiba, dawa, na mashine za uchunguzi, lengo likiwa ni kuhakikisha damu salama inapatikana kwa wote wanaohitaji.

Mkoa wa Ruvuma una jumla ya vituo 37 vinavyotoa huduma ya damu, kati ya hivyo 26 vinamilikiwa na serikali, 11 vinamilikiwa na taasisi za dini, hali inayochochea upatikanaji wa damu salama na ya kutosha. Mbano alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wanafunzi wa shule, vyuo, taasisi za dini, mashirika ya kiraia, na jamii kwa ujumla kuendelea kuchangia damu.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dr. Chioma Mhako, alibainisha kwamba, kati ya Juni 1 hadi 13, 2025, mkoa umekusanya chupa 1,213 za damu, idadi inayovuka lengo la chupa 1,035 kwa kipindi hicho. Dkt. Mhako aliwashukuru wananchi kwa moyo wa huruma na mshikamano wa kuokoa maisha ya wenzao.

 Mafanikio haya ya Mkoa wa Ruvuma ni kielelezo cha umoja, upendo na mshikamano wa jamii, pale inapoungana kwa lengo la kuokoa uhai wa binadamu. Huu ni wito kwa mikoa mingine kuiga mfano wa Ruvuma, na kwa Watanzania wote kuendelea kuchangia damu, kwani tone moja la damu linaweza kuokoa maisha ya mtu aliye hatarini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAKULIMA Ruvuma waomba soko la mahindi kufunguliwa haraka

    June 16, 2025
  • SERIKALI ,dini na wananchi Ruvuma waungana kudumisha amani

    June 16, 2025
  • RUVUMA yaandika historia chupa 4040 za damu zakusanywa kuokoa maisha

    June 15, 2025
  • NAMTUMBO yaagizwa kuongeza kasi ya kushughulikia hoja za CAG

    June 15, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.