• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yamwaga mamilioni kuboresha barabara vijijini mkoani Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: June 14th, 2025

Serikali, kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoani Ruvuma, imetenga mamilioni ya shilingi kwa ajili ya ukarabati wa barabara muhimu zinazounganisha maeneo ya uzalishaji, hususan yale yanayolima kahawa, lengo likiwa ni kurahisisha usafirishaji wa mazao kwenda sokoni. Hatua hiyo inatarajiwa kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wakulima na jamii nzima ya mkoa wa Ruvuma.

 Kaimu Meneja wa TANROADS mkoani Ruvuma, Mhandisi Fedinand Mdoe, alisema barabara ya Nyoni-Mpapa-Mkenda, yenye urefu wa kilometa 108.52, inakarabatiwa kwa Sh milioni 421.26, ambapo kilometa 80.52 zinafanyiwa matengenezo ya kawaida. Aliongeza kuwa kilometa 27 ziko kwenye matengenezo makubwa, ikiwemo kingo za madaraja 3, kwa gharama ya Sh milioni 763.37, na ujenzi wa makalavati 2 unaogharimu Sh milioni 288.05.

Mdoe amezitaja, barabara nyingine zinazofanyiwa matengenezo ni Nyoni-Mpapa-Maguu (kilometa 30) na Mbinga-Mkiri. Alifafanua kuwa, kwenye barabara hiyo, maeneo korofi na miinuko yanawekewa lami ili kuboresha usafiri wa wananchi wa Mbinga na Nyasa. Pia, barabara ya Mbambabay-Lituhi inafanyiwa ukarabati wa dharura, hususan eneo la Lwika, takribani kilometa 15 kutoka Mbambabay, ambapo tuta linainuliwa, box kalavati linajengwa, na changarawe inamwagwa.

Kadhalika, Mdoe alisema barabara ya Nang’ombo-Chiwindi inafanyiwa matengenezo ya dharura kwa kuweka kifusi, lakini changamoto ni magari mazito ya makaa ya mawe, yanayotumia daraja la chuma, jambo linalohatarisha uimara wa daraja hilo. Alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wamiliki wa malori kuzingatia uzito wa mizigo, ili kulinda miundombinu hiyo muhimu. “Tunawasihi makampuni ya makaa ya mawe kuzingatia sheria, kutozidisha uzito wa magari yao, na waangalie maslahi ya umma, si faida yao pekee.” alisema Mdoe.

Kaimu Meneja huyo alihitimisha kwa kusema, kazi nyingi za barabara zinatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu wa fedha, na chache zilizosalia, zilizopewa kipaumbele, zitaendelea hadi Septemba 2025. Hatua hizi zinathibitisha azma ya Serikali ya kuboresha miundombinu ya barabara, kuchochea maendeleo ya kiuchumi, na kuboresha maisha ya wananchi wa Ruvuma.
Ukarabati wa barabara hizi ni chachu ya maendeleo, si tu kwa wakulima wa kahawa na makaa ya mawe, lakini kwa jamii nzima ya mkoa wa Ruvuma.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RUVUMA yaandika historia chupa 4040 za damu zakusanywa kuokoa maisha

    June 15, 2025
  • NAMTUMBO yaagizwa kuongeza kasi ya kushughulikia hoja za CAG

    June 15, 2025
  • RC RUVUMA ahimiza kuongeza kasi kushughulikia Hoja za CAG

    June 14, 2025
  • SERIKALI yamwaga mamilioni kuboresha barabara vijijini mkoani Ruvuma

    June 14, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.