• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatenga bilioni 216 kwa ajili ya chanjo ya mifugo

Imewekwa kuanzia tarehe: July 6th, 2025

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetenga shilingi bilioni 216 kwa ajili ya zoezi la utoaji wa chanjo na utambuzi wa mifugo katika mikoa yote nchini kwa kipindi cha miaka mitano.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Agnes Meena, ametoa taarifa hiyo wakati wa kushuhudia utoaji wa chanjo kwa mifugo katika shamba la Jenista Mhagama lililopo Kijiji cha Mpandangindo, Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma, ikiwa ni kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha utoaji wa chanjo kwa mifugo.

Amesema kuwa zoezi la utoaji wa chanjo ni endelevu na kwamba chanjo hizo zimetolewa na Serikali kwa ruzuku, hivyo ni salama kwa matumizi, akiwahimiza wafugaji kujitokeza kwa wingi kuchanja mifugo yao ili kuepuka magonjwa hatari kwa mifugo.

Bi. Meena ameongeza kuwa Serikali imelenga kuchanja ng’ombe milioni 19 au zaidi, mbuzi na kondoo milioni 17 au zaidi, pamoja na kuku wa kienyeji milioni 40 au zaidi ifikapo Septemba 2025, ikiwa lengo ni kuboresha afya ya mifugo, kuongeza kipato cha wafugaji na kuchangia katika uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Magonjwa Yanayovuka Mipaka kutoka Wizara hiyo, Dkt. Daniel Mdetele, amesema kampeni hiyo inalenga kukabiliana na magonjwa yanayoathiri uzalishaji na biashara ya mifugo.

Amezitaja chanjo zinazotolewa kuwa ni dhidi ya homa ya mapafu ya ng’ombe, sotoka kwa mbuzi na kondoo, pamoja na chanjo ya 3-in-1 kwa kuku wa kienyeji inayodhibiti mdondo, ndui na mafua ya ndege kwa wakati mmoja.

Naye Katibu wa Chama cha Wafugaji Mkoa wa Ruvuma, Prisca Kaponda, amesema wafugaji wa mkoa huo wako tayari kushiriki kikamilifu katika zoezi la chanjo na utambuzi wa mifugo yao.

Vilevile Ndugu Jumanne Mwankhoo, akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, amesema wanaamini kuwa kila mfugaji atafikiwa katika kampeni hiyo ili kuhakikisha mifugo yote inapata chanjo stahiki.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KISIWA cha Lundo Almas iliyojificha ziwa Nyasa

    July 07, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 216 kwa ajili ya chanjo ya mifugo

    July 06, 2025
  • RC RUVUMA akabidhi mkataba wa ujenzi masoko ya Songea

    July 06, 2025
  • CHIFU aliyezikwa akiwa ameketi Mbinga miaka 140 iliyopita

    July 04, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.