• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

USIYOYAJUA kuhusu Chifu aliyezikwa katika kaburi la mviringo akiwa ameketi Mbiinga

Imewekwa kuanzia tarehe: June 8th, 2025

Na Albano Midelo 

Katika kijiji cha Mbuji kilichojificha kwenye vilima vya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, kuna kaburi la aina yake  kaburi linalobeba historia ya maumivu, ujasiri, usaliti, na ushindi.

 Hili si kaburi la kawaida. Ni kaburi la Jemedari wa vita, Mtawala wa kwanza wa kabila la Wamatengo, Chifu Kayuni Kapitangana Ndunguru Makita, ambaye si tu alipigana vita vya ukombozi dhidi ya Wangoni, bali pia aliuawa kikatili na kisha kuzikwa akiwa amekalishwa  katika kaburi la mviringo kama ishara ya heshima kuu kwa mashujaa waliotangulia.

Hii ni hadithi ambayo haijasimuliwa sana, lakini inayobeba uzito mkubwa wa historia ya makabila ya Kusini mwa Tanzania  hadithi ya kiongozi aliyekuwa zaidi ya mtawala; alikuwa ngao ya taifa lake.

MIAKA YA MOTO NA MAPAMBANO

Ilianza mwaka 1824 hadi 1885. Chifu Makita akiwa kijana mwenye ujasiri na hekima ya ajabu, alitokea kuwa kiongozi wa mapambano makali kati ya Wamatengo na Wangoni – kabila lililovamia kutoka Kusini mwa Afrika na kujaribu kutwaa maeneo ya Kusini mwa Tanzania.

 Makita hakusita,alikusanya vijana mashujaa, akawatayarisha, na kuwaongoza kwenye vita vikali vilivyodumu kwa miaka mingi.

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Ngwatura Ndunguru Afisa Wanyamapori Mstaafu na Mbunge Mstaafu wa Mbinga,Chifu Makita alikuwa siyo tu kiongozi wa kijeshi, bali pia mfanyabiashara mwenye ushawishi mkubwa. Kipaji chake cha kipekee cha kuongoza kilimfanya kuwa tishio kwa maadui na tegemeo kwa jamii yake.

"Alikuwa Amiri Jeshi Mkuu wa vita. Hakuanza kama chifu, bali mashujaa waliomzunguka walimtambua kwa uwezo wake wa kipekee wa kuongoza na kushinda vita," anasema Ndunguru.

USALITI NA KIFO CHA KISHUJAA

Baada ya ushindi mkubwa dhidi ya Wangoni katika eneo la Litembo, Makita alionekana kuwa tishio hata kwa washirika wake wa kibiashara.

 Waarabu waliokuwa wakishirikiana na baadhi ya makundi ya Kingoni. Katika kile kilichoaminika kuwa mpango wa usaliti, mwarabu mmoja ambaye alikuwa askari wa kukodi alikata kichwa cha Makita kwa ghafla, kwa hila na tamaa ya mamlaka.

Hicho kichwa kilichokatwa kilikimbizwa mbali na maadui kama ishara ya udhalilishaji wa kiongozi mkubwa wa Wamatengo. Lakini historia haikuishia hapo.

SHUJAA MWANAMKE NA UKOMBOZI WA KICHWA

Katika simulizi inayoshangaza na kuamsha hisia za uzalendo, mama mmoja jasiri kutoka jamii ya Wamatengo alijitokeza.

Alijulikana kwa jina la Kingengi  mwanamke aliyekuwa akiaminika kuwa na uwezo wa kiroho usio wa kawaida. Kwa ujanja na ujasiri, aliwafuata wale waliokuwa na kichwa cha Chifu Makita. Akiwa amejificha nyuma ya vicheko na michezo ya kitamaduni, alifanikiwa kuiba kichwa hicho kutoka kwa maadui waliokuwa wamelewa usingizi.

Usiku huo huo, wazee wa kijiji walikusanyika. Kwa heshima ya shujaa wao, walikiunganisha kichwa na kiwiliwili cha Makita, wakamkalisha kama ilivyo desturi ya maziko ya heshima ya juu, na kumzika kwa siri kubwa kijijini Mbuji.

Na si hilo tu vijana sita waaminifu, mashujaa waaminifu waliompenda Chifu wao, walizikwa hai pamoja naye kama ilivyoaminika kwamba mtu mkubwa hawezi kuzikwa peke yake bila watu wa kumhudumia “ng’ambo ya pili”.

URITHI ULIOFICHIKA, URITHI UNAOSUBIRI KUSIMULIWA

Leo, miaka zaidi ya 140 baadaye, kaburi hilo limesimama Mawe yaliyotumika kujenga kaburi hilo, kwa mujibu wa Ndunguru, yalipangwa kwa heshima maalum, kwa kushirikisha familia na viongozi wa kijiji, mwaka 2004 alipokuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga.

"Historia ya Wamatengo bado haijaandikwa vizuri. Serikali inapaswa kushirikiana na baraza la mila la wamatengo kuhakikisha simulizi hizi hazipotei. Maeneo kama haya yana thamani kubwa ya kihistoria na utalii wa kiutamaduni," anashauri Ndunguru.

Hadithi ya Chifu Makita si ya huzuni tu, bali ni mwito wa kuamka. Ni sauti ya historia inayoibuka kutoka kaburini ikitaka kusimuliwa.

Katika enzi ya sasa ambapo mataifa mengi yanainua hadhi ya mashujaa wao wa kale, Mbinga nayo inayo hadithi ya kutisha na ya kishujaa  hadithi ya mtu aliyezikwa akiwa ameketi, huku vijana sita wakijitolea maisha yao kumsindikiza.

Ni wakati wa Serikali, wanahistoria, na wazalendo kuifukua historia hii. Kwa sababu kama kuna kiongozi ambaye anastahili heshima ya kitaifa kwa ujasiri na mapambano ya kulinda mila na ardhi ya wazawa, basi huyo si mwingine bali ni Chifu Makita  shujaa asiyeweza kufutika katika kumbukumbu za Ruvuma, Tanzania, na Afrika nzima.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAKULIMA Ruvuma waomba soko la mahindi kufunguliwa haraka

    June 16, 2025
  • SERIKALI ,dini na wananchi Ruvuma waungana kudumisha amani

    June 16, 2025
  • RUVUMA yaandika historia chupa 4040 za damu zakusanywa kuokoa maisha

    June 15, 2025
  • NAMTUMBO yaagizwa kuongeza kasi ya kushughulikia hoja za CAG

    June 15, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.