Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Marco G. Chilya, kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Camillus Wambura, amewapandisha vyeo askari 155 waliohitimu mafunzo ya upandishaji vyeo kwa mwaka 2024/2025.
Hafla hiyo ya kihistoria imeambatana na pongezi kwa askari hao waliofaulu kwa mafanikio na kuhitimisha mafunzo yao kwa ufanisi mkubwa.
Sherehe ya uvalishwaji wa vyeo hivyo imefanyika kwenye viwanja vya Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Ruvuma, ambapo imehudhuriwa na maafisa waandamizi, wakaguzi pamoja na askari kutoka vitengo mbalimbali vya jeshi hilo.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Kamanda Chilya amewataka askari waliopandishwa vyeo kuhakikisha wanayathamini na kuyatendea haki madaraka mapya waliyopewa.
Ametoa wito kwao kuwahudumia wananchi kwa uadilifu, weledi na kwa kufuata misingi ya haki, kama alivyoelekeza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchin
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.