• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA Ruvuma waomba soko la mahindi kufunguliwa haraka

Imewekwa kuanzia tarehe: June 16th, 2025

Wakulima wa mahindi mkoani Ruvuma wamesisitiza ombi lao kwa Serikali kufungua soko la mahindi haraka, ili waepuke hasara inayoweza kuwakumba kutokana na bei duni inayotolewa na wafanyabiashara wa mitaani.

Wamesema Serikali, kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), ndiyo mkombozi wa pekee wa wakulima, kwani hununua mahindi kwa bei nzuri kati ya Shilingi 500 hadi 700 kwa kilo  ikilinganishwa na wafanyabiashara binafsi wanaotoa Shilingi 300 hadi 400 tu, bei inayowadidimiza kiuchumi.

John Nchimbi, mkulima wa kijiji cha Matiri, Wilayani Mbinga, alisema kuchelewa kufunguliwa soko la NFRA kunawaumiza, kwani wafanyabiashara wa mitaani wameshaanza kuwanunulia mahindi shambani kwa bei ya hasara.

 “Tunaiomba Serikali ifungue soko haraka ili tusipate hasara, wafanyabiashara wanazunguka mashambani na kununua kwa bei ya chini. Hii si haki kwetu,” alisema Nchimbi.

Erasto Mapunda wa Magagura, aliongeza kuwa ucheleweshaji wa soko una athari si tu kiuchumi, lakini pia kiafya na kimaisha, kwani familia nyingi zinategemea mahindi kama kitega uchumi.

 Naye Sebastian Komba wa Lukarasi, aliitaka NFRA kuzingatia jiografia ya Wilaya ya Mbinga, hususan kata nane zinazozalisha mahindi kwa wingi, kama Mkako, Kigonsera, Amanimakolo, Namswea, Muungano, Matiri, Lukarasi, na Ruanda.

Amesema kuwa Kituo cha Kigonsera pekee hakiwezi kuhudumia wakulima wote, kwani umbali wa kusafirisha ni mrefu, na gharama zinawakandamiza.

Takwimu za NFRA kanda ya Songea zinaonesha kwamba, kwa mwaka wa fedha 2024/2025, lengo la ununuzi wa mahindi lilikuwa tani 72,000, lakini hadi Desemba 2024, NFRA ilinunua tani 118,292, sawa na asilimia 164.3 ya lengo, na akiba ya mahindi ilifikia tani 196,498,737.



Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAKULIMA Ruvuma waomba soko la mahindi kufunguliwa haraka

    June 16, 2025
  • SERIKALI ,dini na wananchi Ruvuma waungana kudumisha amani

    June 16, 2025
  • RUVUMA yaandika historia chupa 4040 za damu zakusanywa kuokoa maisha

    June 15, 2025
  • NAMTUMBO yaagizwa kuongeza kasi ya kushughulikia hoja za CAG

    June 15, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.