Wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wametakiwa kuzingatia mbinu bora za uvunaji wa mahindi ili kupunguza upotevu wa mazao na kuhakikisha ubora wa mavuno unadumu hadi sokoni.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Ndugu Frank Sungau, alisema mahindi yanapaswa kuvunwa yakiwa yamekomaa vizuri na kukauka kwa kiwango kinachotakiwa.
Alifafanua dalili kuu za mahindi yaliyokomaa ni magunzi kuanza kuinama chini na majani ya mabua kunyauka.
Sungau alisisitiza umuhimu wa kuvuna mapema punde tu mahindi yanapokomaa, ili kuepuka hasara inayoweza kusababishwa na mvua za ghafla, wadudu, au wanyama waharibifu.
Alitahadharisha kwamba kuchelewa kuvuna kunawaweka wakulima hatarini kupoteza sehemu ya mavuno yao.
Aidha, aliwataka wakulima kutouza holela mahindi yao, bila kuzingatia mahitaji ya familia zao kwa mwaka mzima.
“Kila kaya inapaswa kuhesabu idadi ya wanachama wake, ihakikishe inabaki na akiba ya kutosha kwa chakula, kisha ziada ndiyo iuzwe,” alisisitiza Sungau.
Wakati huo huo, Sungau alibainisha kwamba Serikali inajiandaa kuanza rasmi ununuzi wa mahindi kwa msimu wa 2025/2026. Hatua hiyo inatarajiwa kutoa soko la uhakika kwa wakulima, kuimarisha kipato chao, na kuleta unafuu wa bei kwa jami
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.