• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAFISA Habari wapewa nguvu mpya,Mchengerwa afungua milango ya mapinduzi ya mawasiliano

Imewekwa kuanzia tarehe: May 24th, 2025

Katika kikao kazi maalum kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Dodoma, Mji wa Serikali Mtumba, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ametoa maagizo makubwa kwa Maafisa Habari wa Mikoa, Halmashauri na Taasisi chini ya OR-TAMISEMI, akisisitiza kuwa wao ni kiungo muhimu katika kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya nchi. 

Akizungumza  kwenye kikao kazi hicho, Mchengerwa amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri na makatibu Tawala wa mikoa  kuhakikisha Maafisa Habari wanapewa nafasi ya kushiriki kikamilifu kwenye kila hatua ya maendeleo.

Mchengerwa ameweka bayana kuwa Maafisa Habari si watazamaji bali ni sehemu ya timu ya maendeleo, hivyo lazima wahusishwe katika ziara za viongozi, tathmini za miradi na kikao chochote rasmi.

 “Maafisa Habari wakiwa na uelewa mpana wa yanayotekelezwa, watakuwa na nguvu ya kusambaza habari sahihi kwa umma na kuijenga Serikali kwa msingi wa uwazi,” amesema Waziri huyo kwa msisitizo.

Katika kuhakikisha weledi wa Maafisa Habari unaimarishwa, Mchengerwa ametoa agizo kwa Wakurugenzi na Makatibu Tawala kuandaa mafunzo kazini kwa watumishi hao, yakiwemo uandishi wa takwimu, ubunifu wa infographics, uhariri wa video, na maudhui mengine ya kisasa ya mawasiliano. 

Aidha, ametilia mkazo umuhimu wa kuwahusisha Maafisa Habari katika vikao vyote vya kisheria na kuwawezesha kuwa sehemu ya menejimenti rasmi.

Waziri Mchengerwa pia amewataka viongozi wa Mikoa na Halmashauri kuhakikisha kila Afisa Habari anapatiwa ofisi yake, bajeti maalum ya uendeshaji, na kushirikishwa katika kuratibu vipindi vya televisheni na redio vinavyoitangaza Serikali. “Fedha zipo, lakini hazitumiwi ipasavyo kwenye mawasiliano. Hili halikubaliki,” alisisitiza kwa ukali.

Kwa upande wao, Maafisa Habari wametakiwa kuandaa Mpango Kazi unaoendana na vipaumbele vya taasisi zao, kuwasilisha taarifa za utendaji kila baada ya miezi mitatu, na kuwa wabunifu katika uchakataji na usambazaji wa habari. 

Waziri amesisitiza kuwa mitandao ya kijamii na tovuti rasmi ni nyenzo kuu ya kufikisha taarifa kwa wananchi, hivyo inapaswa kuhuishwa kila wakati.

Kikao hicho kimeweka msingi wa mageuzi makubwa katika mfumo wa mawasiliano ya Serikali, huku Mchengerwa akisisitiza kuwa kila Afisa Habari anapaswa kuwa “shujaa wa simulizi ya maendeleo”. 

Ametaka taarifa zote za miradi ya maendeleo zifuatiliwe kwa karibu ili wananchi wapate taarifa sahihi za utekelezaji wa miradi yao. “Tumeingia zama mpya – zama za Serikali ya uwazi, uwajibikaji na mawasiliano yenye mvuto kwa umma,” amehitimisha.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI yatoa maelekezo kuimarisha utoaji taarifa kwa umma

    May 25, 2025
  • NGORO siri ya kilimo kinachotunza ardhi kwa miaka 300

    May 25, 2025
  • MAAFISA Habari wapewa nguvu mpya,Mchengerwa afungua milango ya mapinduzi ya mawasiliano

    May 24, 2025
  • SERIKALI ilivyodhamiria kuboresha mabweni na madarasa wilayani Tunduru

    May 24, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.