• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAMTUMBO ilivyodhamiria kuboresha huduma za afya vijijini

Imewekwa kuanzia tarehe: August 1st, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, Ndg. Philemon Mwita Magesa, ameongoza ziara ya ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa vituo viwili vya afya katika vijiji vya Mchomolo na Mgombasi, wilayani humo.

Miradi hiyo yenye thamani ya jumla ya shilingi milioni 508, inatekelezwa na mkandarasi DMC Contractor Limited, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuboresha huduma za afya katika maeneo ya pembezoni.

Mradi huo unatekelezwa kwa mujibu wa mkataba ulioanza tarehe 1 Julai 2025, na unatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba 2025, ndani ya kipindi cha miezi mitatu. Ujenzi katika kituo cha afya cha Mchomolo unagharimu shilingi milioni 258, wakati ule wa Mgombasi ukigharimu shilingi milioni 250.

Fedha hizo zimetolewa na Serikali kupitia bajeti ya maendeleo ya sekta ya afya, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora na za karibu.

Katika vituo hivyo vinavyojengwa, miongoni mwa majengo yanayojengwa ni pamoja na jengo la huduma ya wagonjwa wa nje (PPD), pamoja na miundombinu mingine muhimu kama maabara, wodi za wagonjwa, nyumba za watumishi na vyoo vya kisasa. Mkurugenzi Magesa ameweka bayana kuwa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kupunguza vifo vinavyotokana na kukosa huduma ya afya kwa wakati, hasa kwa akina mama na watoto vijijini.

Akiwa katika ukaguzi huo, Mkurugenzi Magesa aliwataka wakandarasi kuhakikisha wanazingatia viwango vya kitaalamu, muda wa utekelezaji, na ubora wa kazi kwa mujibu wa mkataba. “Serikali haitakubali mzaha kwenye miradi ya afya, tunahitaji kazi bora, kwa wakati, ili wananchi waanze kunufaika haraka iwezekanavyo,” alisisitiza Magesa mbele ya wananchi, viongozi wa vijiji na wataalamu wa afya waliokuwepo katika ziara hiyo.

Wananchi wa vijiji husika wameonesha furaha yao kwa maendeleo ya ujenzi huo, wakieleza kuwa wamekuwa wakitembea zaidi ya kilomita 15 kufuata huduma za afya katika maeneo ya mbali, hali iliyokuwa ikiathiri hasa wazee, wajawazito na watoto. "Tunamshukuru sana Rais Samia kwa kutuletea kituo cha afya, tumeumia sana kwa miaka mingi," alisema Bi. Theresia Nyagawa, mkazi wa Mchomolo.

Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo inaendelea kutekeleza mikakati ya kuongeza vituo vya afya na hospitali katika kata mbalimbali ili kufikia lengo la kila kata kuwa na kituo cha afya ifikapo mwaka 2027. Tayari halmashauri hiyo ina vituo vya afya vinavyofanya kazi 11 na vingine vinne vikiwa katika hatua za ujenzi, ikiwa ni ongezeko la zaidi ya  asilimia70 tangu mwaka 2020.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MUHOGO wa Nyasa ulivyopamba maonesho ya nanenane Mbeya

    August 02, 2025
  • RAIS SAMIA azindua mradi mkubwa wa Urani Namtumbo

    August 01, 2025
  • WATENDAJI Mbinga watakiwa kutekeleza miradi ya maendeleo

    August 01, 2025
  • RC RUVUMA asikiliza kero za wafanyabiashara soko la Bombambili Songea

    August 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.