• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKUMBUSHO ya vita ya Majimaji kubadilishwa

Imewekwa kuanzia tarehe: June 18th, 2025

Makumbusho ya mashujaa wa Vita ya  Majimaji Songea, mkoani Ruvuma, yanatarajiwa kubadilika sura, kutoka sanamu za kawaida kwenda sura halisi za mashujaa walioshiriki vita hiyo, hatua inayolenga kuwakumbuka kwa uhalisia zaidi.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Makumbusho na Mali Kale Makumbusho ya Taifa, Adelaide Sallema, wakati wa kikao chake na wajumbe wa Baraza la Makumbusho na Machief wa Songea.

Alifafanua kuwa lengo ni kuutambulisha mradi wa uumbaji upya wa sanamu 12 za mashujaa wa Majimaji, ili zifanane na sura halisi za wahusika.

Sallema alibainisha kwamba mradi huo wa uboreshaji una lengo la kuhifadhi historia ya Vita ya  Majimaji kwa uhalisi, kuleta mvuto wa kipekee wa utalii wa kihistoria, na kuimarisha urithi wa kitamaduni wa Taifa.

Aliongeza kwamba mabadiliko haya yatawasaidia wageni, wanafunzi, na jamii ya Kitanzania kuijua vyema historia ya mashujaa wa Majimaji.

Kikao hicho, kilichofanyika viwanja vya Makumbusho ya Majimaji Songea, kilihudhuriwa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akiwemo Mhadhiri na Mkuu wa Makumbusho Kanda ya Kusini Nyanda za Juu, Frola Vicent.

Wataalamu hao walishirikiana kutoa maoni ya jinsi mradi huo utakavyotekelezwa.

Maboresho haya yanatarajiwa kuleta sura mpya ya Makumbusho ya Majimaji Songea, yakiboresha mvuto wa utalii wa kihistoria, kuhamasisha umma kuuthamini urithi wa taifa, na kutoa fursa kwa vizazi vijavyo kujifunza historia ya mashujaa wa Majimaji kupitia taswira halisi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAKUMBUSHO ya vita ya Majimaji kubadilishwa

    June 18, 2025
  • WAKULIMA Songea watakiwa kuvuna mahindi kwa mbinu bora

    June 17, 2025
  • RUVUMA walivyoadhimisha siku ya mtoto wa Afrika

    June 17, 2025
  • RUVUMA yaadhimisha siku ya mtoto wa Afrika kwa kishindo,serikali,jamii na wazazi waungana kumlinda mtoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.