• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA aiagiza Manispaa ya Songea kutekeleza Hoja za CAG

Imewekwa kuanzia tarehe: June 14th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, ametoa maelekezo kwa wakuu wa idara na vitengo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika kuandaa majibu ya hoja na mpango kazi wa utekelezaji wa mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Akizungumza katika Baraza Maalum la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2023/24, Kanali Ahmed amesisitiza uwajibikaji na kuchukua hatua stahiki dhidi ya watumishi watakaobainika kusababisha hasara au hoja kwa uzembe.

Ameitaka menejimenti ya Manispaa ya Songea kuhakikisha taarifa za mwisho wa mwaka zinaandaliwa kwa kuzingatia viwango vya kihasibu vya kimataifa katika sekta za umma, huku wakifuata sheria, kanuni, na taratibu za fedha na manunuzi ili kuepuka hoja zisizo za lazima na kudhibiti uwezekano wa hoja kujirudia kila mwaka.  

Pamoja na hayo, ametoa maagizo ya kushughulikia hoja 14 za miaka ya nyuma pamoja na maagizo mawili ya LAAK ambayo hayajatekelezwa kikamilifu, akisisitiza kuwa hoja hizo lazima zikamilike na kuwasilishwa kabla ya Septemba 30, 2025.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mary Makondo, amepongeza usimamizi mzuri wa fedha za umma kwa mwaka wa fedha 2023/24, ambapo halmashauri zote za mkoa wa Ruvuma zimepata hati safi kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Amesema mafanikio hayo ni matokeo ya weledi, uadilifu, na uzalendo wa timu za wataalamu, wakiongozwa kwa umakini na madiwani, wakurugenzi wa halmashauri, pamoja na sekretarieti ya mkoa, jambo ambalo linaendelea kuimarisha uwajibikaji na ufanisi katika usimamizi wa rasilimali za umma.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea, Mheshimiwa Michael Mbano, ameonyesha dhamira thabiti ya kushughulikia hoja mbalimbali zinazoikabili Manispaa hiyo, licha ya changamoto zinazohitaji bajeti na muda wa utekelezaji.

Pamoja na juhudi hizo, amebainisha kuwa anajivunia mafanikio makubwa katika kuongeza mapato ya Manispaa, ambapo kiwango kimepanda kutoka Bilioni 2.5 hadi kufikia kati ya Bilioni 9-10 kwa mwaka.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RUVUMA yaandika historia chupa 4040 za damu zakusanywa kuokoa maisha

    June 15, 2025
  • NAMTUMBO yaagizwa kuongeza kasi ya kushughulikia hoja za CAG

    June 15, 2025
  • RC RUVUMA ahimiza kuongeza kasi kushughulikia Hoja za CAG

    June 14, 2025
  • SERIKALI yamwaga mamilioni kuboresha barabara vijijini mkoani Ruvuma

    June 14, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.