• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI ,dini na wananchi Ruvuma waungana kudumisha amani

Imewekwa kuanzia tarehe: June 16th, 2025

Viongozi wa dini, serikali na waumini wa madhehebu mbalimbali mkoani Ruvuma wameungana katika ibada maalum ya maombi ya siku saba, wakiombea amani, umoja na mshikamano wa Tanzania, hususan wakati huu wa mabadiliko makubwa ya kijamii na kisiasa.

Akihudhuria ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Pentecostal Hema ya Makutano, kijiji cha Namtuhi, Halmashauri ya  wilaya ya Songea, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abass Ahmed, aliwakilishwa na Afisa Utamaduni wa Mkoa, Anthony Luoga,alisisitiza wajibu wa kila raia kulinda amani ya taifa, akibainisha kuwa amani ni tunu adimu, inayopotea kwa urahisi lakini ni ghali sana kuirudisha.

“Kulinda amani ya taifa letu ni jukumu la kila mmoja. Amani ni tunu tuliyopewa, lakini si rahisi kuipata tena pindi inapotoweka. Tushirikiane sote kuilinda, tuishabikie, na tuirithishe kwa vizazi vijavyo,” alisema Luoga, akihamasisha umma kudumisha umoja, upendo na mshikamano.

Aliwataka wazazi na walezi kuzingatia malezi bora, hususan ya kidini, ili kuzuia wimbi la vijana wanaotumia mitandao ya kijamii kutoa maneno ya matusi, kejeli, na dharau, hususan dhidi ya viongozi wa dini, kisiasa na jamii. Alisisitiza kuwa, malezi mazuri yanaleta raia wema, wanaoheshimu madaraka, taratibu na utawala wa sheria.

Akizungumza katika ibada hiyo, Askofu wa Kanisa la Pentecostal  Hema ya Makutano, Javery Eliakimu, alisema ibada hiyo ni sehemu ya siku saba za maombi ya kuliombea taifa, viongozi wa serikali, na jamii kwa ujumla. Alibainisha kuwa lengo ni kuwaombea viongozi wafanye uamuzi wa busara, wa haki, na wa maendeleo, huku wakiimarisha umoja wa kitaifa.

“Jukumu letu kama viongozi wa dini si kuhukumu, wala kuchochea chuki, bali ni kuliombea taifa na viongozi wake. Tukiungana, tutaijenga Tanzania imara, yenye amani, umoja na maendeleo ya kweli,” alisema Askofu Eliakimu, akihimiza waumini kuendelea kuliombea taifa, viongozi wake na jamii.

Maombi hayo yameshirikisha waumini, viongozi wa dini, wazee wa kanisa, viongozi wa serikali ya mkoa, na wananchi wa kawaida, ambao walijitokeza kwa wingi, kuonyesha mshikamano wa kidini, umoja na upendo wa taifa. Ikumbukwe, Kanisa la Pentecostal Hema ya Makutano limeandaa mfululizo wa ibada kama hizi, zinazolenga kuimarisha amani, umoja, na maendeleo ya Tanzania.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAKULIMA Ruvuma waomba soko la mahindi kufunguliwa haraka

    June 16, 2025
  • SERIKALI ,dini na wananchi Ruvuma waungana kudumisha amani

    June 16, 2025
  • RUVUMA yaandika historia chupa 4040 za damu zakusanywa kuokoa maisha

    June 15, 2025
  • NAMTUMBO yaagizwa kuongeza kasi ya kushughulikia hoja za CAG

    June 15, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.