• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MISITU ya vijiji inavyoibadilisha Ruvuma kuwa ngome ya kijani ya uchumi mpya

Imewekwa kuanzia tarehe: July 16th, 2025

 Katika Halmashauri za  wilaya za Madaba, Mbinga, Tunduru, Songea na Namtumbo mkoani Ruvuma, mapinduzi ya kiuchumi yanaendelea kuota mizizi kupitia usimamizi shirikishi wa misitu ya vijiji, maarufu kama CBFM (Community-Based Forest Management).

Charles Meshack ni  Mkurugenzi, TFCG akizungumza kwenye utambulisho wa mradi wa FORLAND mkoani Ruvuma anasema ni mageuzi yanayoweka jamii mbele katika usimamizi wa rasilimali, wakati huohuo yakiweka msingi wa maendeleo endelevu yanayoakisi dira ya Tanzania ya kijani.

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2023, zaidi ya shilingi bilioni 5 zilipatikana kupitia uvunaji endelevu wa mbao kutoka misitu inayosimamiwa na jamii mkoani Ruvuma na Lindi pekee. Fedha hizi zimeelekezwa katika huduma muhimu kama afya, elimu, miundombinu na usimamizi wa misitu, na kuonesha kuwa misitu ni chanzo cha matumaini.

Vijiji 26 Vyajitosa Rasmi Kuimarisha Misitu yao

Kupitia mradi wa kimataifa wa FORLAND unaogharimu zaidi ya Euro milioni 20.8, vijiji 26 katika Mkoa wa Ruvuma vimechaguliwa kushiriki kwa kina katika uanzishaji wa Hifadhi za Misitu ya Vijiji (VLFRs) na kupewa mafunzo maalum ya usimamizi wa misitu.

Mradi huu, unaofadhiliwa na Serikali ya Finland kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania, una lengo la kuimarisha uwezo wa jamii katika uzalishaji wa mbao, usimamizi wa moto, matumizi bora ya ardhi na kuibua fursa kwa biashara ndogondogo kupitia misitu.

Kwa sasa, asilimia 92 ya misitu kwenye ardhi ya vijiji haijalindwa, hali inayoonesha dharura ya kuongeza maeneo chini ya CBFM ili kukabiliana na ukataji hovyo wa misitu unaofikia hekta 600,000 kwa mwaka kitaifa.

 FORLAND inalenga kubadilisha taswira hii kwa kutumia mbinu shirikishi, elimu, na teknolojia endelevu.

 Misitu Inayozalisha Kipato: Mbao, Mkaa, na  Kaboni

Mbali na mbao, baadhi ya vijiji mkoani Ruvuma sasa vimeanza kuzalisha mkaa endelevu kwa kutumia vitalu vya mzunguko wa miaka 24, na teknolojia za tanuri bora zinazolinda mazingira. Hii si tu inasaidia mazingira, bali pia inaleta mapato yanayotumika kulipia huduma za kijamii.

Mbali na hilo, miradi ya kimataifa kama REDD+ imeanza kulipa vijiji kwa kulinda misitu. Mfano wa kuigwa ni mradi wa Ntakata uliopatikana mapato ya USD milioni 5.7 kwa jamii mwaka 2023. Ruvuma, ikiwa na misitu mingi ya vijiji, ina nafasi kubwa ya kunufaika zaidi na miradi hii endapo vikwazo vya kisheria na kisera vitatatuliwa.

 Misitu ni msingi wa uchumi wa vijiji

Wakati dunia inaendelea kuelekea kwenye uchumi wa kijani na uzalishaji endelevu, Ruvuma inajipambanua kuwa mfano hai wa mafanikio ya usimamizi wa misitu unaoongozwa na wananchi. FORLAND si mradi wa kupanda miti tu, bali ni mapinduzi ya fikra, sera na uongozi wa kijamii.

Akizungumza kwenye utambulisho wa mradi huo kwenye ukumbi wa Mipango Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Songea,Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Dr.Lous Chomboko ameupongeza mradi wa FORLAND kwa kudhamiria kukuza uchumi na kupunguza umasikini kwa wananchi vijijini kupitia mazao ya misitu.

Amesisitiza FORLAND wanapotekeleza mradi huo kuwashirikisha kikamilifu wananchi vijijini katika Halmashauri saba zinazoshiriki mradi huo katika Mkoa wa Ruvuma hali ambayo itawajengea uelewa wananchi na  kuwekeza zaidi katika CBFM kama mkakati mkuu wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MISITU ya vijiji inavyoibadilisha Ruvuma kuwa ngome ya kijani ya uchumi mpya

    July 16, 2025
  • DC NAMTUMBO awapongeza mashujaa wa uhifadhi

    July 16, 2025
  • SASA ni zamu yenu kusoma kwa bidiii-DC Tunduru

    July 16, 2025
  • MAWE yanayovutia wengi Mkowela Tunduru

    July 15, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.