• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI inatambua mchango wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali

Imewekwa kuanzia tarehe: June 25th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amesema Serikali inatambua mchango wa mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGOs) katika kuchochea maendeleo katika Jamii, mkoa na Taifa kwa ujumla.

Ameyasema hayo wakati akisoma hotuba yake kwenye Mkutano wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Ruvuma uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

"Ninatambua kazi kubwa mnayoifanya ya kushirikiana na Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi katika nyanja mbalimbali, niwapongeze na niwaombe muendelee kutupa ushirikiano katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazofanyika katika mkoa wetu," alisema Kanali Ahmed.

Kanali Ahmed ameyataka mashirika hayo kuhakikisha wanashirikiana vizuri na mamlaka za Serikali ikiwa ni pamoja na Wilaya, Halmashauri, pamoja na watendaji wa Kata na Tarafa, katika utekelezaji wa shughuli zao, lengo ni kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza, na kuhakikisha kuwa mipango yao inatambulika rasmi na taasisi husika za Serikali.

Naye Mwenyekiti wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Ruvuma (NaCoNGO), Anthony Mbilinyi, amesema wajibu wa mashirika yasiyo ya Kiserikali ni kutoa huduma bora na stahiki katika jamii, kufuatilia sera na kuhamasisha mabadiliko ya kijamii na kuhakikisha shughuli zote zinazofanywa na mashirika hayo zinaendeshwa Kwa kuzingatia Sheria na maadili ya kitaifa na kimataifa.

Ametaja mafanikio ya mashirika hayo katika Mkoa wa Ruvuma kuwa ni kuwafikia wananchi wapatao 76,000 kupitia afua mbalimbali ambazo zimekuwa kichocheo cha maendeleo ya mkoa na kuboresha ustawi wa jamii ikiwa zaidi ya shilingi bilioni 2 zimetumika katika wilaya zote za mkoa kutekeleza miradi ya afya, kilimo, na maendeleo ya kijamii.

Kwa upande wake Msajili Msaidizi wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Ruvuma, Xsaveria Mlimila, amesema katika Mkoa wa Ruvuma mashirika 192 yamesajiliwa kisheria na changamoto kubwa ni kukosekana kwa taarifa sahihi za mashirika hayo ambayo yamesajiliwa kisheria.

Amebainisha kuwa kwa mwaka wa fedha 2024/2025 mashirika hayo katika mkoa wa Ruvuma yamekuwa yakiendelea kutekelezeka miradi mbalimbali ya kijamii,  kiuchumi na kiafya katika afua mbalimbali ikiwemo Elimu, lishe, kilimo, afya, mazingira pamoja na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia ambapo walengwa 89,000 wamefikiwa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIWANDA kikubwa cha mbolea kitakachowanufaisha wakulima Ruvuma chazinduliwa

    June 29, 2025
  • RAS Ruvuma ateta na viongozi wa NHIF

    June 26, 2025
  • CHACHA amekabidhi ofisi Masanja Tunduru

    June 26, 2025
  • RC RUVUMA atembelewa na viongozi wa Bima ya Afya

    June 26, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.