• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TAARIFA ya Wakala wa Hifadhi ya Chakula Kanda ya Songea NFRA

Posted on: December 29th, 2022

7.1 WAKALA WA HIFADHI YA CHAKULA KANDA YA SONGEA (NFRA)

Taarifa ya utekelezaji wa kazi za wakala wa hifadhi ya chakula – NFRA kuanzia Julai 1, 2022 hadi 30 Novemba 2022

i.          Ununuzi Msimu wa 2022/2023

Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kupitia kanda ya Songea ilipangiwa kununua jumla ya tani 25,000 za mahindi. Kutokana na upatikanaji mdogo wa nafaka kwa msimu huu wa 2022/2023 kanda ilipewa idhini ya kununua tani 6000 kwa kuanzia. Aidha, kuanzia tarehe 21 Septemba, 2022 kanda ilipewa idhini ya kununua tani 3000 za nyongeza ili kuendelea na zoezi la kuongeza akiba ya chakula kwa ajili ya kukabiliana na majanga mbalimbali.

ii.         Njia za Ununuzi Zilizopagwa

Kutokana na ushindani katika soko kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Wakala ulipanga kutumia njia kuu tatu za ununuzi ambazo ni:-

i)          Kununua kwa njia ya vituo vya ununuzi

ii)         Kununua kwa njia ya vikundi vya wakulima vya ushirika.

iii)        Kununua kwa kutumia mawakala.

iii.        Mpango wa Ununuzi

Wakala ulipanga kiwango cha ununuzi kwa Halmashauri saba zilizopo Mkoa wa Ruvuma kwa kuzingatia uwiano wa taarifa za matarajio ya uzalishaji wa ziada ya mahindi. Aidha, kutokana na upatikanaji mdogo wa nafaka kwa mwaka huu, mgawanyo huo haukufuatwa.

iv.        UNUNUZI

Kanda ya Songea ilianza ununuzi katika maeneo yote ya Mkoa wa Ruvuma kuanzia tarehe 05/08/2022 na mpaka kufikia tarehe 30/11/2022, kanda ilikuwa imenunua tani 7,098.283 zenye thamani ya shilingi 5,168,367,960/= kutoka katika vituo vya ununuzi vya kudumu 11 na vile vya muda 5 pia ununuzi ulifanyika kupitia mawakala 6 na kuleta jumla ya vituo 22.

V.        Bei za Ununuzi

Mahindi yalinunuliwa kwa bei kati ya shilingi 650 na 780. Mabadiliko ya bei za kununulia zilibadilika mara kwa mara kutokana na ushindani wa bei zilizokuwa sokoni. Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) ulifanya mabadiliko ya bei ili kuongeza akiba ya Taifa ya chakula kwa lengo la kuihakikikishia Nchi inakuwa na uhakika wa chakula kukabiliana na majanga mbalimbali hasa ukame uliojitokeza katika baadhi ya maeneo ya nchi.

vi.        Mafanikio

a)         Hadi kufikia tarehe 30 Novemba 2022, NFRA ilikuwa imefanikiwa kununua tani 7098.283 za mahindi sawa na asilimia 28.4 ya tani 25,000 zilizopangwa kununuliwa katika msimu wa 2022/2023.

b)         Serikali kupitia NFRA iii nufaisha wakulima kwa kuongeza bei ya kununulia mahindi kadri wafanyabiashara walivyoongeza bei sokoni hadi kufikia kikomo cha bei ya shilingi 780 kwa kila kilo hivyo kuwasaidia wakulima kujiingizia kipato cha kununulia p na kurudi shambani.]

c)         Kutengeneza ajira kwa vijana takribani 450 waliotumika kwenye zoezi la ununuzi

d)         Kusaidia serikali kukusanya kodi ya zuio yenye jumla ya shilingi 103,367,359.20 ambapo hadi Novemba 30 2022 kiasi cha shilingi 69,997,898 kilikuwa kimelipwa kwa kamishina wa TRA. Aidha jumla ya shilingi 155,051,038.80 Kitalipwa kwa Halmashauri kama ushuru wa mazao (crop ces).

vii.       Changamoto

Ufinyu wa nafaka ya mahindi sokoni kwa msimu huu wa 2022/2023 kulikosababishwa na mahitaji ya nafaka ya mahindi kuwa kubwa sana.

NFRA kutumia muda mrefu kununua tani 7098.283 tu ukilinganisha na misimu mingine hivyo, kuongeza gharama za uendeshaji

Baadhi ya wakulima/ wafanyabiashara kuleta    vituoni nafaka           ambazo hazikizi viwango vya ubora.

viii.      Hitimisho

Mwisho, Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula unaishukuru Serikali kwa ujumla kuwezesha kutekeleza jukumu la ununuzi wa mahindi kwa kutenga fedha za kutosha kununua mahindi ya wakulima kwa njia mbalimbali.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.