• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Madaba ilivyotumia bilioni tatu kutekeleza mradi wa jengo la Halmashauri

Imewekwa kuanzia tarehe: July 7th, 2020

SERIKALI ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli imetoa zaidi ya shilingi bilioni tatu kutekeleza mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kamati ya Siasa ya CCM ya Mkoa wa Ruvuma,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Kassim Mpenda amesema mradi ulianza kutekelezwa mwaka 2017  na kwamba lengo la mradi ni kutatua changamoto ya uhaba wa ofisi unaowakabili watumishi wa Halmashauri hiyo na wananchi.

Hata hivyo amesema mradi unaendelea kujengwa kwa awamu tatu hadi sasa ambapo katika awamu ya kwanza mkataba ambao ulikuwa unatekelezwa na Mkandarasi Wakala wa Majengo Tanzania TBA,ulikuwa ni zaidi ya shilingi milioni 493,awamu ya pili ni mkataba wa zaidi ya bilioni mbili na  awamu ya tatu ujenzi unafanyika kwa force akaunti kwa ajili ya umaliziaji  wa asilimia 18 iliyobakia kukamilisha mradi.

“Mradi huu hadi sasa umepokea zaidi ya sh.bilioni tatu kutoka serikali kuu,kiasi cha zaidi ya sh. Bilioni  1.9 kimekwishatumika katika jengo hili,Mkandarasi TBA katika awamu zote mbili amelipwa zaidi ya bilioni 1.89’’,alisema Mpenda.

Hata hivyo amesema Mkandarasi TBA alisimamishwa kuendelea na kazi ya ujenzi  na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina  Mndeme Juni 6 mwaka huu,baada ya Mkandarasi huyo kupata changamoto ya kufungiwa akaunti zake zote na kushinda kuendelea na kazi,hali iliyosababisha Halmashauri kutumia force akaunti kukamilisha mradi huo.

Amesema mradi wa jengo hilo hivi sasa upo katika hatua za umaliziaji ukiwa umefikia asilimia 82 kwa ujumla wake na kwamba mradi unatarajia kukamilika Agosti 30 mwaka huu.

Akizungumza mara ya kutembelea na kukagua mradi huo kwa niaba ya Kamati,Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho ameushauri uongozi wa Halmashauri hiyo kufanya kazi mchana na usiku ili kukamilisha kazi kwa sababu mradi huo umechelewa kukamilika na wananchi wanausubiri kwa hamu.

“Sisi Chama cha Mapinduzi tunataka wakati wa Kampeni Agosti mwaka huu tuwaambie wananchi wa Madaba kuwa tuliahidi,tumetekeleza kujenga jengo la Halmashauri,mkichelewa mtatuangusha’’,alisema Mwisho.

Hata mwisho kwa niaba ya wananchi wa Madaba amemshukuru Rais Magufuli kwa kutoa fedha ambazo zinatekeleza mradi huo mkubwa wa ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Madaba ambalo likikamilika litatatua changamoto kwa wananchi na watumishi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Julai 5,2020

Madaba

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.