• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Songea yapokea zaidi ya bilioni tatu kutekeleza miundombinu ya elimu

Imewekwa kuanzia tarehe: June 14th, 2023

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma imepokea zaidi ya shilingi bilioni tatu kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya elimu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Neema Maghembe amesema kati ya fedha hizo  Halmashauri imepokea fedha zaidi ya shilingi milioni 149 kupitia Ufadhili wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (Tanzania Education Authority- TEA) kwaajili ya ujenzi wa bweni la wasichana lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 120.

Amesema Halmashauri hiyopia imepokea fedha kiasi cha shilingi milioni 362.2 kutoka katika kampuni ya Barrick Gold Mine Tanzania kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika shule ya sekondari Maposeni.

Maghembe amesema fedha hizo zitatumika kujenga madarasa manne ambapo kila darasa litagharimu shilingi milioni 24.

Ameongeza kuwa fedha hizo pia zitajenga mabweni mawili ambapo kila bweni litagharimu shilingi milioni 128  na ujenzi wa matundu ya vyoo sita ambapo kila tundu litagharimu kiasi cha shilingi milioni 1.7.

“Kampuni ya Barrack imetoa fedha hizo ili kuunga mkono jitihada na juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuboresha elimu nchini’’,alisema.

Hata hivyo amelitaja lengo la ujenzi wa miundombinu hiyo kuwa ni kuwezesha wanafunzi waliofaulu kujiunga na kidato cha tano mwaka 2023, kupata fursa ya kuendelea na masomo.

Kulingana na Mkurugenzi huyo,Halmashauri  hiyo pia imepokea fedha kiasi cha shilingi milioni 834 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya kuongeza miundombinu ya wanafunzi wa kidato cha tano katika shule ya sekondari Jenista Mhagama.

Amesema  fedha hizo zitatumika kujenga madarasa 12 ambapo kila darasa litagharimu fedha kiasi cha shilingi milioni 24,mabweni manne ambapo kila bweni litatumia  kiasi cha shilingi milioni 128 na ujenzi wa matundu ya vyoo 20 ambapo tundu moja litagharimu shilingi milioni 1.7.

Amesema Halmashauri hiyo pia imepokea fedha kiasi cha shilingi milioni 751.8 kutoka Serikali kuu kaajili ya kuongeza miundombinu ya wanafunzi wa kidato  cha tano katika shule ya sekondari Mpitimbi.

Amesema fedha hizo zitatumika kujenga madarasa tisa ambapo kila darasa litagharimu shilingi milioni 24,ujenzi wa mabweni manne ambapo kila bweni litagharimu shilingi milioni 128 na ujenzi wa matundu ya vyoo 14 ambapo tundu moja litagharimu milioni 1.7.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa  Halmashauri  ya Wilaya ya Songea Mheshimiwa Menas Komba  ameishukuru Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mhe. Jenista Joakim Mhagama kwa kuendelea kuimarisha miundombinu ya elimu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.