• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma umefunguka

Imewekwa kuanzia tarehe: September 8th, 2022

NYASA KUWA KANDA MAALUM YA KIUCHUMI KATIKA USHOROBA WA MTWARA

SERIKALI inatarajia kuanzisha Kanda Maalum ya kiuchumi {Special Economic Zone}  katika eneo  la Mbambabay ziwa Nyasa  Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma ili kuhakikisha bidhaa zote ambazo zinapatikana Kariakoo jijini Dar es salaam ziweze kupatikana Nyasa.

Hayo yamesema na Balozi wa Tanzania nchini Malawi Mheshimiwa Humphrey Polepole alipofanya ziara ya siku moja  mkoani Ruvuma katika wilaya ya Nyasa kuangalia fursa za uwekezaji katika ushoroba wa Mtwara,unaonzia mkoani Mtwara hadi Mbambabay ziwa Nyasa.

Akizungumza baada ya kukagua bandari Kongwe ya Mbambabay na bandari mpya ya Ndumbi ambayo serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 12 kujenga bandari hiyo,Balozi Polepole  ametoa rai kwa wadau kuwa tayari kutumia fursa zote zinazopatikana katika ushoroba wa Mtwara.

“Ushoroba huu ni wa barabara inayotoka bandari ya Mtwara na inakuja kwa kilometa 822 mpaka bandari ya Mbambabay,ushoroba huu katika kusini mwa Afrika,ndiyo ushoroba bora zaidi na  mfupi kuliko shoroba nyingine zote’’,alisema.

Amesema ushoroba wa Mtwara umesheheni madini ya aina mbalimbali yakiwemo makaa ya m awe,dhahabu,uranium na madini mengine ambayo ni fursa kwa wakazi wa eneo lote la ushoroba.

Polepole amesema wamedhamiria kuhakikisha ushoroba wa Mtwara unatangazwa na kuwa mbadala wa ushoraba wa Dar es salaam kwa sababu Dar es salaam hadi Lilongwe ni Kilometa 1600 wakati Ushoroba wa Mtwara ni kilometa 900.

Balozi huyo wa Tanzania nchini Malawi amesema kutokana na hali hiyo ametoa rai kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania TBA kuboresha miundombinu ya bandari ziwa Nyasa ili serikali ivune pesa na  kukusanya kodi kwenye ushoroba huu kutoka nchi za Malawi,Msumbiji,Zambia na Zimbabwe.

Amesema serikali ina mipango mikubwa ya kuwezesha usafirishaji wa shehena ya mizigo zaidi ya tani laki moja  ambayo itawezesha milango ya kibiashara kufunguka katika bandari za Mtwara,Mbambabay,na ushoroba wote wa Mtwara.

Ametoa katika nchi ya Malawi tayari ubalozi umepokea maombi ya wafanyabiashara ambao wapo tayari  kujiridhisha utayari wa ushoroba wa Mtwara ili waanze kupitisha shehena za mizigo kupitia ushoroba wa Mtwara.

”Sisi kama ubalozi wa Malawi,tumetoa ombi maalum kwa Mkoa wa Ruvuma hususan wilaya ya Nyasa,kuhakikisha  tunaanzisha eneo maalum la kiuchumi ambalo linawezesha kupatikana  bidhaa zote ambazo zinapatikana Kariakoo jijini Dar es salaam ziweze kupatikana Mbambabay’’,alisisitiza.

Amesema ili kuhakikisha suala hilo linafanikiwa kwa asilimia 100,meli ya abiria ya Mbeya II katika ziwa Nyasa hivi karibuni inatarajia kuanza safari za kuvuka ziwa kutoka Bandari ya  Mbambabay Tanzania na Kwenda nchini Malawi katika bandari za Ntakabay,Chilumba na Chipoka ambako watafarishwa wafanyabiashara na mizigo kuja Mbambabay na kununua bidhaa mbalimbali zitakazokuwepo  baada ya kuwa kituo cha kiuchumi.

Amesema bidhaa hizo zitakwenda nchini Malawi hadi Bandari ya Tete nchini Msumbiji kupitia ziwa Nyasa ambayo itakuwa ni  fursa kubwa ya kibiashara  wa Tanzania nan chi jirani.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas  akizungumzia uwekezaji uliofanyika katika bandari ya  Ndumbi,amesema serikali imewekeza mabilioni ya fedha kutekeleza mradi huo ambao umekamilika.

Amesema Mkoa umejiandaa kuanzisha maeneo maalum kwa ajili ya uwekezaji ambapo hivi sasa bidhaa zote ambazo zitahitajika katika nchi Jirani  zitapatikana katika bandari ya Mbambabay ziwa Nyasa ili kupunguza umbali wa Kwenda Dar es salaam.

Ametoa rai kwa wafanyabiashara wa Tanzania kuchangamkia fursa hiyo na kwamba serikali ipo tayari kuwawezesha miundombinu yote inayohitajika ili bidhaa zote ziweze kupatikana katika wilaya ya Nyasa.

 Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbinga ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mheshimiwa Aziza Mangasongo amesema kukamilika kwa mradi wa bandari ya Ndumbi kunafungua fursa mpya za uwekezaji mkoani Ruvuma.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ruvuma

Septemba 8,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.