• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma aagiza stakabadhi ghalani kutumika kuuza mazao ya wakulima

Imewekwa kuanzia tarehe: June 21st, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amewaagiza viongozi na wadau wa vyama vya ushirika kusimamia mapato ya Halmashauri kupitia mazao yanayouzwa kwa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa lengo la kuongeza maduhuli ya Serikali.

 RC  Ibuge ametoa maagizo hayo wakati wa kikao cha baraza la madiwani, cha kujadili Hesabu za Mkaguzi Mkuu wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/2020, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

 Amesema kuwa, mapato ya Serikali yamekuwa yanapotea kwasababu ya usimamizi na ufuatiliaji mdogo, kwa baadhi viongozi kutosimamia ipasavyo mazao yanayopaswa kuuzwa  kwa mfumo wa stakabadhi ghalani ,kitendo  kinachosababisha Halmashauri kukusanya chini ya kiwango kilichokusudiwa

Amesisitiza kuwa Waheshimiwa madiwani na watendaji kusimamia kwa umakini mkubwa uuzaji na ununuzi wa mazao ya wakulima, ili waweze kuuza mazao hayo kwa bei yenye tija, ili wakulima waweze kunufaika na kilimo wanacholima badala ya kulanguliwa mazao yao na walanguzi na kusababisha kuvunjika moyo kwakukosa mwelekeo.

 ”Mazao yanauzwa kwa stakabadhi ghalani yatauzwa  kwa mfumo huo kwakuwa ni mwongozo uliowekwa na serikali”,amsisitiza Balazi Ibuge.

Ameongeza kwa kusema kuwa usimamizi na ufuatilia soko la mnada wa stakabadhi ghalani, unasaidia serikali kukusanya mapato na wakulima kuuza mazao kwa bei yenye tija na faida kwao. 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, wamesema wanakubaliana na mfumo huo wa stakabadhi ghalani unaowataka wakulima wa ufuta soya na mbaazi kuuza mazao hayo kwenye vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS)

“Hatupingani na maamuzi ya serikali ila tunataka viwepo vituo vidogo vidogo vya kukusanyia mazao hayo na soko lifanyike mara mbili kwa wiki badala ya siku moja kwa wiki”, walisema wakulima hao.

Wamesema changamoto wanayokutana nayo katika mfumo huo ni kutembea umbali mrefu, gharama za kukodi vyombo vya usafiri kwa ajili ya kufikisha mizigo kwenye vyama  vya msingi vya ushirika pamoja na kufanyika kwa mnada mara moja kwa wiki.

 Kufuatia changamoto hiyo wameiomba serikali kuweka vituo vidogo vidogo vya kukusanyia mazao, karibu na maeneo   kitendo ambacho kitawaondolea adha ya kutembea umbali mrefu, gharama za kukodi vyombo vya usafiri kwa lengo la kufikisha mazao, kwenye vyama  vya ushirika sanjari na kuacha tabia ya kwenda kuuza mazao yao kwa walanguzi.

Mfumo wa stakabadhi ghalani ni mfumo ambao unawataka wakulima na wanunuzi kuuza mazao ya ufuta soya na mbaazi, kuuza mazao yao kwenye soko la mnada kwa bei ya makubaliano baina ya mnunuzi na mfanyabishara.

Imeandikwa na

Jacquelen Clavery

Afisa Habari Songea DC

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.