• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI azindua matumzi sahihi ya mbolea Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: July 25th, 2024

MATUMIZI ya mbolea  hapa nchini,yameongezeka kutoka  wastani wa tani 363,599 katika msimu wa kilimo 2021/202 hadi kufikia tani 840,714 kwa msimu wa kilimo 2023/2024.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa mbolea Tanzania Joel Lauren amesema hayo jana,wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha usajili wa wakulima na matumizi sahihi ya mbolea uliofanyika wilayani Mbinga.

Amesema,Mkoa wa Ruvuma ambao ni kati ya Mikoa ya kimkakati ya uzalishaji wa chakula hapa nchini, kwa miaka ya karibuni umeongoza kwa matumizi ya mbolea ambapo msimu 2022/2023 Mkoa huo ulitumia  zaidi ya tani 83,472.

“katika msimu 2023/2024 mkoa wa Ruvuma umetumia tani 100,000,hivyo kuendelea kuwa kinara kwa matumizi ya mbolea na kuwa miongoni mwa mikoa tegemezi katika uzalishaji wa chakula hapa nchini”amesema.

Laurent alitaja mikoa inayofuatia kwa matumizi ya mbolea ni Njombe tani 75,358,Mbeya tani 75,252,Songwe tani 71,230 na mkoa wa Iringa ambao umetumia tani 44,214.

Amesema,matumizi ya mbolea kwa sasa ni muhimu kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu kunakohitaji ongezeko la uzalishaji wa chakula ili kukidhi mahitaji,ukuaji wa miji,miundombinu na huduma za kijamii zinazochangia kupunguza eneo linalofaa kwa kilimo.

Ameeleza kuwa,matumizi sahihi ya mbolea kunaongeza tija na kuchangia kukuza kipato cha mkulima mmoja mmoja,ukuaji wa sekta ya kilimo na pato la Taifa kwa ujumla.

Ameongeza kuwa,hapa nchini kuna mbolea za viwandani na mbolea za asili ambazo zinatumiwa na wakulima,lakini changamoto ni matumizi kidogo ya mbolea kwa baadhi ya maeneo kunatokana na dhana potofu kwamba mbolea inaharibu ardhi na baadhi ya wakulima kukosa elimu ya matumizi sahihi ya mbolea”alisema Laurent.

Amewakumbusha wakulima umuhimu wa kutumia mbolea katika uzalishaji wa mazao kwenye mashamba yao kwani unasaidia  kurutubisha,kuboresha afya ya udongo na kuzalisha mazao kwa wingi katika eneo dogo.

Kwa upande wake  Naibu Waziri wa Nishati Mheshmiwa  Judith Kapinga amesema,sekta ya kilimo ndiyo mhimili wa uchumi wa Tanzania na inaajiri takribani theluthi mbili ya nguvu kazi ya Taifa na inachangia asilimia 65 ya malighafi za viwandani,asilimia 100 ya usalama wa chakula na zaidi ya asilimia 26 ya pato la Taifa.

Kapinga amesema,katika mazingira ambayo kilimo ndiyo  sekta ya uchumi,maendeleo ya mwananchi na Taifa kwa ujumla yanategemea zaidi ufanisi katika sekta hiyo.

Amesema,Serikali ya awamu ya sita imedhamira kufanya mapinduzi  makubwa katika sekta ya kilimo kwa kuongeza bajeti ya wizara kutoka takrbani Sh.bilioni 294 mwaka 2021/2022 hadi kufikia  Sh.trilioni 1.24 kwa mwaka 2024/2025.

Amewataka wakulima hapa nchini wakiwemo wa wilaya ya Mbinga na mkoa wa Ruvuma,kuchangamkia fursa zinazotolewa na Serikali kwa kujisajili katika mfumo wa kidijitali kupitia Ofisi za Watendaji wa vijiji na mitaa.

Naibu Waziri Kapinga amesema,kujisajili kwenye mfumo wa kidijitali kutawaweza wakulima kununua mbolea kwa gharama nafuu,kuongeza uzalishaji,kuboresha maisha yao na kuchangia ukuaji wa uchumi.

Ametaja faida nyingne kwa wakulima kujisajili  kwenye mfumo wa kidijitali,ni kuiwezesha serikali kupata takwimu sahihi zitakazotumika kuweka mipango ya kuwaendeleza wakulima,sekta ya kilimo na kupata huduma za ugani,taarifa za masoko na huduma za kifedha kupitia kanzidata.

Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Ruvuma Jumanne Mankhoo,ameipongeza mamlaka ya udhibiti wa ubora wa mbolea kwa kusimamia vema upatikanaji wa pembejeo za ruzuku iliyosaidia kupatikana kwa wingi na kwa urahisi katika meneo mengi ya mkoa huo.

Naye Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Ndani na Ununuzi wa Mbolea kwa pamoja wa TFRA Dkt Louis Kasera amesema,kampeni hiyo inalenga kuhamasisha wakulima kote nchini juu ya matumizi sahihi ya mbolea ili waweze kongeza uzalishaji.

Amewahakikisha wakulima kuwa,mpango wa mbolea za ruzuku utaendelea kutolewa hadi katika msimu wa kilimo 2024/2025 na kuwataka wakulima waongeze juhudi na kutumia mbolea kwenye shughuli zao za kilimo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.