• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAMTUMBO ilivyoandikwa katika ramani ya Dunia

Imewekwa kuanzia tarehe: July 31st, 2025

Katika tukio la kihistoria lililoshuhudiwa na maelfu ya wananchi, viongozi wa kitaifa, na wadau wa kimataifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Julai 30, 2025, ameandika ukurasa mpya wa maendeleo kwa kuzindua Kiwanda cha Majaribio cha Kuchenjua Urani kilichopo katika eneo la Mkuju River, Wilaya ya Namtumbo, Mkoa wa Ruvuma.


Mradi huo wa kipekee, unaosimamiwa na kampuni ya Mantra Tanzania Limited kwa ushirikiano na kampuni ya kimataifa ya Rosatom kutoka Urusi, unatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi mikubwa zaidi ya kimkakati si tu kwa Tanzania bali kwa Afrika Mashariki nzima. 

Kiwanda hicho ni hatua ya mwanzo kuelekea uzalishaji mkubwa wa urani nchini – madini yenye mchango mkubwa katika sekta ya uzalishaji wa nishati ya nyuklia duniani.

“Leo tunashuhudia mwanzo wa enzi mpya ya kimaendeleo nchini – Tanzania sasa inaingia rasmi katika orodha ya mataifa yenye uwezo wa kuchakata na kutumia madini ya kimkakati kwa ustawi wa watu wake na maendeleo ya sayansi, teknolojia na diplomasia ya nishati,” alisema Dkt. Samia huku akishangiliwa na umati uliofurika katika eneo hilo la Mkuju River.

MWELEKEO WA MAGEUZI YA UCHUMI NA NISHATI

Kwa mujibu wa taarifa rasmi, mradi huu una thamani ya Shilingi Trilioni 3.06 na unatarajiwa kuanza uzalishaji rasmi mwaka 2026. 

Mbali  na kuchochea uchumi wa taifa, urani itatumika kama chanzo cha kuzalisha umeme wa nyuklia, hali itakayosaidia kupunguza utegemezi wa vyanzo vya kawaida vya nishati na kuiweka Tanzania kwenye ramani ya nchi zenye uwezo wa kuzalisha nishati endelevu kwa karne zijazo.

Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde, alibainisha kuwa mradi huu utafungua fursa nyingi kwa Watanzania, hususan vijana wa maeneo ya kusini mwa nchi kupitia ajira, uhamishaji wa teknolojia, na mafunzo ya kitaalamu ya usimamizi wa rasilimali za kimkakati.

“Uchimbaji wa urani si jambo la kawaida. Ni sekta ya juu yenye mahitaji makubwa ya utaalamu, ulinzi na ufuatiliaji wa kimataifa. Ndiyo maana tunahakikisha kwamba wazawa wanajengewa uwezo wa kisayansi na kiufundi kuendesha shughuli hizi kwa usalama na ufanisi,” aliongeza Waziri Mavunde.

URANI YA TANZANIA: AKIBA NA FURSA

Tanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika zenye akiba kubwa ya madini ya urani. Kwa mujibu wa Wizara ya Madini, urani imeshathibitishwa kuwapo katika maeneo mbalimbali ya nchi ikiwemo Bahi, Galapo, Minjingu, Mbulu, Simanjiro, Ziwa Natroni, Manyoni, Tunduru, Songea, Madaba, Nachingwea, na hususan Mkuju River wilayani Namtumbo.

Mara baada ya kuanza kwa uzalishaji katika mradi huu wa Mkuju River, Tanzania inatarajiwa kuwa nchi ya tatu barani Afrika kwa uzalishaji wa urani – nyuma ya Niger yenye akiba ya tani 200,000 na Namibia yenye tani 100,000. Niger, ambayo ndiyo kinara wa uzalishaji wa urani Afrika, ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa dunia.

ATHARI CHANYA ZA MRADI KWA RUVUMA NA TANZANIA KWA UJUMLA

Kwa Mkoa wa Ruvuma, hii ni hatua kubwa ya kuibua fursa mpya za uwekezaji, uboreshaji wa miundombinu, biashara ndogondogo, pamoja na uimarishaji wa elimu ya sayansi na mazingira. Pia, mradi huu unatarajiwa kuwa kichocheo kikuu cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Wilaya ya Namtumbo na maeneo jirani.

Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Mhe. Vita Kawawa, hakuficha furaha yake akieleza kuwa ujio wa Rais Samia sio tu umetimiza ndoto ya muda mrefu ya wananchi wa Namtumbo bali umechochea matumaini mapya kwa vizazi vijavyo.

“Tunamshukuru Rais wetu kwa dhamira thabiti ya kulifikisha taifa kwenye uchumi wa viwanda kwa vitendo. Namtumbo sasa si historia tena – ni kitovu cha nishati ya Afrika Mashariki,” alisema kwa hisia kubwa.

Uzinduzi wa Kiwanda hiki ni alama ya mwanzo wa safari ya Tanzania kuelekea kuwa taifa linalotumia rasilimali zake kwa ufanisi, kwa maendeleo ya watu wake, bila kuathiri mazingira wala usalama 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TANZANIA yaanza safari mpya ya kisayansi,Rais Samia azindua kiwanda cha urani Namtumbo

    July 31, 2025
  • KIWANDA cha majaribio ya kuchenjua Urani kilichozinduliwa na Rais Samia Namtumbo

    July 31, 2025
  • WANANCHI wakimsikiliza Rais Samia Likuyu Namtumbo

    July 31, 2025
  • ENZI mpya katika sekta ya madini wilayani Namtumbo

    July 31, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.