• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RAIS SAMIA azindua mradi wa urani Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: July 30th, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema mradi wa kiwanda cha majaribio cha kuchenjua madini aina ya urani katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma unaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi chache barani Afrika zinazochakata na kuongeza thamani  rasilimali zake ndani ya nchi.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Likuyu mara baada ya kuzindua mradi huo, Mhe. Dkt. Samia amebainisha kuwa Afrika inashikiliwa na asilimia 20 ya hifadhi ya madini aina ya urani na ni asilimia ndogo tu inayochakatwa ndani ya bara la Afrika.

"Tanzania itakuwa kwenye ramani ya duniani kama moja kati ya wachangiaji 10 wakubwa wa malighafi hii muhimu ya nishati safi, mradi huu wa majaribio ni sehemu ya utekelezaji wa dira yetu ya kuifanya Tanzania kuwa Taifa lenye viwanda na kufikia matarajio ya uchumi wa kati ngazi ya juu unaojitegemea,"alisema Mhe. Rais Dkt. Samia.

Ameeleza kuwa kiwanda hicho cha majaribio ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati ya Serikali ya kuhakikisha madini hayo yanatumika kwa manufaa ya watanzania wote kwa kuzingatia usalama wa kiafya, kimazingira na kufuata viwango vya kimataifa.

Amesema tathimini iliyofanywa inaonyesha kuwa mradi huo itakuwa na uhai wa uzalishaji kwa zaidi ya miaka 20 na katika kipindi hicho Tanzania itapata faida mbalimbali ikiwemo uwekezaji wa fedha za kigeni unaokadiriwa kufikia dola za kimarekani bilioni 1.2 ( zaidi ya Trilioni 3 za kitanzania) na ajira kati ya 3,500 mpaka 4,000 huku ajira za kudumu zikiwa 750.

Mhe. Rais Dkt. Samia ameitaka kampuni inayotekeleza mradi huo ambayo ni Mantra Tanzania kuzingatia ushirikishwaji wa watanzania na wajibu wa kampuni kwa jamii ambapo amewataka kutoa ajira kwa watanzania hususan waliopo katika vijiji na eneo la karibu na mradi kwa ajira ambazo hazihitaji ujuzi mkubwa.

Kwa upande wake, Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde, amesema kuwa uzinduzi wa mradi huo ni hatua ya awali kuelekea ujenzi wa mtambo mkubwa wa uchenjuaji wa madini ya urani, akisisitiza kwamba katika nchi za Afrika Mashariki na Kati, hakuna mradi mwingine wa aina hiyo unaotarajiwa kujengwa wilayani Namtumbo.

Ameeleza kuwa mtambo huo utaiwezesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi tano pekee barani Afrika zinazomiliki mradi mkubwa wa uchenjuaji wa madini ya urani.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amesema mradi huo unabeba matumaini makubwa ya mkoa na Taifa kwa ujumla, kwa kuwa unakadiriwa kuwa na mchango mkubwa katika kuongeza pato la Taifa, ajira kwa vijana na kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi hasa katika sekta ya Elimu, Afya na Miundombinu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TANZANIA yaanza safari mpya ya kisayansi,Rais Samia azindua kiwanda cha urani Namtumbo

    July 31, 2025
  • KIWANDA cha majaribio ya kuchenjua Urani kilichozinduliwa na Rais Samia Namtumbo

    July 31, 2025
  • WANANCHI wakimsikiliza Rais Samia Likuyu Namtumbo

    July 31, 2025
  • ENZI mpya katika sekta ya madini wilayani Namtumbo

    July 31, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.