• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANESCO Ruvuma yasambaza umeme vijiji 119

Imewekwa kuanzia tarehe: July 7th, 2021

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO)  mkoani Ruvuma kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA) limefanikiwa kusambaza umeme katika vijiji 119 kati ya lengo la kusambaza umeme vijiji 161.

Meneja wa TANESCO Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Florence Mwakasege amesema mradi huo umetekelezwa kupitia REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza ukihusisha pia ujenzi wa njia mbili za umeme wenye urefu wa Kilometa 106 kuelekea kituo cha kufua umeme wa maji Nakatuta Mto Ruvuma.

Amezitaja gharama za mradi huo kuwa ni zaidi ya shilingi bilioni 43 na kwamba vijiji ambavyo bado havijasambaziwa umeme utekelezaji wake upo katika hatua mbalimbali.Mhandisi Mwakasege amesema tayari wateja 5,902 wa awali wameunganishiwa kati ya lengo la kuunganishiwa wateja 6,178 mradi huo utakapokamilika kwa asilimia 100

Amesema Mkoa wa Ruvuma una jumla ya vijiji 551,kati ya hivyo vijiji vyenye umeme ni 295,vijiji visivyo na umeme vilivyoomba kupitia  REA awamu ya tatu mzunguko wa pili 256 na vijiji vitakavyokuwa na umeme baada ya miradi inayoendelea kukamilika ni 295.

Hata hivyo amesisitiza kuwa hadi kufikia Desemba 2022 vijiji vyote ambavyo havijapatiwa umeme katika Mkoa wa Ruvuma vinatarajiwa kumfikiwa na umeme.

Kuhusu upatikanaji wa umeme mkoani Ruvuma,Mhandisi Mwakasege amesema upatikanaji wa umeme ni wa kuridhisha baada ya Mkoa kuunganishwa na Grid ya Taifa katika Wilaya za Songea,Namtumbo,Mbinga,Nyasa na Tunduru.

“Mkoa wa Ruvuma pia unapata umeme kutoka kwa wawekezaji binafsi wa Kampuni  za Tulila na Andoya ambao wana uwezo wa kufua umeme megawati 5.5 na kuingiza kwenye Grid ya Taifa’’,alisema Mwakasege.

Amewataja wateja waliounganishiwa umeme katika kipindi cha Julai 2020 hadi Machi 2021 kuwa ni 7,411 ukilinganisha na lengo la mwaka la kuunganisha wateja 6,000 sawa na asilimia 123.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 6,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.