• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Tunduru wafurahia uboreshaji huduma za afya

Imewekwa kuanzia tarehe: March 13th, 2024

Baadhi ya wananchi wa Tunduru mkoani Ruvuma,wamempongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri ya kusimamia na kuboresha sekta ya afya ambayo awali ilikabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uchakavu wa majengo,upungufu wa dawa,vifaa tiba na watumishi hasa katika maeneo ya vijijini.

Wameishukuru serikali kwa uamuzi wa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa zahanati, vituo vya afya na Hospitali ya wilaya Tunduru hali iliyowezesha upatikanaji wa huduma bora za matibabu wilayani humo.

Said Halfani alisema,kwa sasa wanafurahi na matumaini makubwa kuona serikali imeamua kutoa fedha ili kuboresha huduma za afya hasa katika Hospitali ya wilaya Tunduru ambayo ni tegemeo kubwa kwa watu wa wilaya hiyo kongwe hapa nchini.

Hussein Yusuf alisema,kabla ya ukarabati wa majengo na ujenzi wa majengo mapya katika Hospitali hiyo ikiwemo jengo la wagonjwa wa dharura hapo awali walilazimika kwenda Hospitali nyingine kama Hospitali ya Misheni Mbesa na Ndanda kwa ajili ya kufuata huduma za dharura ambazo zilikosekana katika Hospitali ya wilaya.

Yusuf licha ya kuipongeza serikali kwa kazi nzuri inayofanya,ameiomba kuhakikisha ukarabati huo unaendeane na utoaji wa huduma bora kwa watu wanaofika kupata matibabu.

Aidha,ameitaka serikali kuhakikisha inawachukulia hatua baadhi ya watumishi wazembe wanaofanya kazi kwa mazoea na wale wanaotoa lugha chafu kwa wagonjwa wanofika kupata huduma.

Halvina Masangano mkazi wa mtaa wa Majengo Tunduru mjini,amefurahishwa na ubora wa majengo mapya,lakini ameiomba serikali kuongeza idadi ya watumishi kwani waliopo ni wachache kutokana na Hospitali hiyo kuwa kimbilio kubwa la wananchi wa wilaya ya Tunduru.

Kwa upande wake mganga mfawidhi wa Hospitali ya wilaya Tunduru Dkt Athuman Mkonoumo alisema,kwa sasa hali ya upatikanaji wa huduma za afya katika Hospitali ya wilaya Tunduru zimeimarika baada ya serikali kutoa Sh.bilioni 1.270 kwa ajili ya kufanya ukarabati wa baadhi ya majengo ya kutolea huduma za afya.

Dkt Mkonoumo alisema,kati ya fedha hizo Sh.milioni 900 zimetumika kufanya ukarabati wa jengo la wagonjwa wa nje(OPD),Maabara na jengo la upasuaji huku Sh.milioni 370 zimefanikisha kujenga jengo jipya la wagonjwa wa dharura(EMD).

Ameishukuru serikali kuwapatia fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo ambayo yamesaidia kuboresha huduma hasa ikizingatiwa kumekuwa na ongezeko kubwa la wateja wanaofika kwenda kupata huduma katika Hospitali hiyo.

Alisema,ukarabati na ujenzi wa majengo hayo ikiwemo jengo la dharura umekamilika kwa asilimia 100 na majengo yote mapya yameanza kutoa huduma,hivyo kupunguza rufaa kwa baadhi ya wagonjwa kwenda nje ya wilaya ya Tunduru kufuata huduma zaidi za matibabu.

Alisema,ukarabati huo umerahisisha utendaji kazi kwa watumishi wa Hospitali kwa sababu ya kuwepo kwa vifaa na miundombinu ya kisasa tofauti na hapo awali ambapo kulikuwa na majengo machache na chakavu.

Ameipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kufanya ukarabati mkubwa wa jengo maalum la upasuaji ambalo limekuwa msaada mkubwa kwa mama wajawazito wanaofika kujifungua kwa njia hiyo ambapo idadi yao inafikia zaidi ya 80 kwa mwezi.

Dkt Mkonoumo alisema,Hospitali ya wilaya Tunduru ni kati ya Hospitali kongwe hapa nchini na kwa muda mrefu haijawahi kufanyiwa ukarabati,kwa hiyo majengo yake mengi yalikuwa chakavu hivyo kukwamisha mkakati wa serikali wa kutoa huduma bora na za kisasa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.