• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATENDAJI Mbinga watakiwa kutekeleza miradi ya maendeleo

Imewekwa kuanzia tarehe: August 1st, 2025

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Joseph Kashushura, ametoa wito mzito kwa Watendaji wa Kata, Watendaji wa Vijiji na Wenyeviti wa Vijiji kushirikiana kwa karibu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa lengo la kuongeza umiliki, kupunguza gharama na kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ubora unaotakiwa.

Rai hiyo imetolewa, wakati wa kikao kazi muhimu kilichowakutanisha Watendaji hao na Timu ya Menejimenti ya Halmashauri katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya utekelezaji wa miradi iliyopokea fedha kutoka Serikali Kuu. "Hii miradi yetu, Serikali imeleta fedha kwa ajili ya utekelezaji. Naomba sana mkahamasishe wananchi kwenye maeneo yenu ili tushirikiane kwa pamoja," alisisitiza Kashushura.

Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa, ili miradi ya maendeleo iwe endelevu, ni lazima wananchi wa maeneo husika washirikishwe kikamilifu tangu hatua za mwanzo. Alisema ushirikiano huo si tu huongeza umiliki wa miradi, bali pia huchochea ari ya wananchi kulinda na kuthamini rasilimali za umma. “Wananchi wakishiriki kwenye miradi, wanakuwa sehemu ya suluhisho, na mara nyingi huchangia nguvu kazi, vifaa na hata ulinzi wa miundombinu,” alisema.

Kwa upande wake, Claudius Miringa, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahilo Asili kutoka Kata ya Mbuji, alionesha kufurahishwa na hatua ya Halmashauri kuitisha kikao hicho muhimu. “Tangu nimechaguliwa sijawahi kushiriki kikao cha aina hii. Hii ni hatua kubwa ya uwajibikaji na ushirikiano. Naahidi kushirikiana kwa karibu na wananchi katika utekelezaji wa miradi,” alisema kwa msisitizo.

Naye Mtendaji wa Kata ya Lukarasi, Joseph Ndunguru, alisema kikao hicho ni chachu ya mabadiliko chanya katika utekelezaji wa miradi. Alisema kimewaongezea maarifa na kuelewa dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanahusishwa moja kwa moja katika miradi yote inayogusa maisha yao. “Kwa mtazamo wangu, huu ndio msingi wa maendeleo shirikishi tunayoyahitaji kwa sasa,” aliongeza.

Takwimu zinaonesha kuwa katika mwaka wa fedha 2025/2026, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imepokea zaidi ya shilingi bilioni 3.8 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara katika kata zaidi ya 15. Fedha hizo zinalenga kuinua huduma za kijamii vijijini, na kushirikisha wananchi kutasaidia utekelezaji kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MUHOGO wa Nyasa ulivyopamba maonesho ya nanenane Mbeya

    August 02, 2025
  • RAIS SAMIA azindua mradi mkubwa wa Urani Namtumbo

    August 01, 2025
  • WATENDAJI Mbinga watakiwa kutekeleza miradi ya maendeleo

    August 01, 2025
  • RC RUVUMA asikiliza kero za wafanyabiashara soko la Bombambili Songea

    August 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.