• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATU wenye ulemavu 812 wamejiriwa serikalini kuanzia 2020 hadi 2023

Imewekwa kuanzia tarehe: June 14th, 2023

WAZIRI wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu kazi,vijana,ajira na watu wenye ulemavu Prof. Joyce Ndalichako,ameziagiza Halmashauri zote hapa nchini kuhakikisha zinatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kununua mahitaji ikiwemo mafuta kinga kwa watu wenye Ualbino.

Waziri  Ndalichako ametoa agizo hilo katika Hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa wilaya ya Songea Kapenjama Ndile,wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya  uelewa kuhusu Ualbino ambayo kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Aidha Waziri Ndalichako alisema,kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali ilitenga Sh.milioni 50 kwa ajili ya mahitaji mbalimbali ikiwemo mafuta kwa watu wenye Ualbino.

Alisema,Serikali imewapa kipaumbele wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na masuala ya elimu na uwezeshaji kichumi,afya,ajira,mafunzo ya ufundi stadi ili waweze kukabliana na changamoto  katika maisha yao.

“Serikali ya awamu ya sita imeendelea na kutekeleza na kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu nchini kwa kuzingatia sera,sheria,mikataba ya kikanda na Kimataifa na itaendelea kufanya hivyo wakati wote”alisema Ndalichako.

Alisema,serikali imeendelea kuboresha huduma za afya kwa kujenga vituo vya kutolea huduma za afya vyenye miudombinu rafiki kwa watu wote wenye ulemavu wa aina mbalimbali.

Mwenyekiti  wa Tume ya haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu,ameitaka Serikali kuongeza juhudi za kuwatambua watu wenye Ualbino na mahitaji yao kwa kutoa tiba na kinga ya saratani ya ngozi na kuweka mazingira mazuri kupitia mfumo wa utoaji wa huduma za afya nchini.

Ameishauri Serikali kupitia vyombo vya ulinzi na usalama, kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika  maeneo mbalimbali ili kuzuia na kuchukua hatua juu ya vitendo vya unyanyasaji dhidi ya watu wenye ualbino.Amewaomba wananchi kushirikiana na serikali  kukemea vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji na kutoa taarifa katika mamlaka husika juu ya vitendo  hivyo dhidi ya watu wenye Ualbino katika maeneo yao.

Alisema,jitihada zaidi zinahitajika ili kuondoa kabisa changamoto za watu wenye Ualbino hususani ugonjwa wa saratani ya ngozi kwani kufanya hivyo kutawezesha ujumuishi wenye uimara wa kufurahi haki za binadamu.

Ameitaka jamii,kuunganisha nguvu kutokomeza saratani ya ngozi kwa watu wenye Ualbino ikiwemo kutoa elimu kwa kupinga vitendo vya udhalilishaji,unyannyasaji na mauaji ya watu wenye Ualbino.

Ametoa wito kwa watu kuachana na imani,mila,desturi na mitazamo potofu ambayo huwafanya watu wenye Ualbino kujiona hawakubaliki,hawawezi na hawana mchango wowote kwa jamii inayowazunguka na Taifa kwa ujumla katika shughuli zinazohusu maendeleo.

Katika hatua nyingine Jaji mstaafu Mwaimu,amewaasa watu wenye Ualbino kuzingatia miongozi ya afya juu ya kujikinga na saratani ya ngozi na kuchukua  hatua za haraka kwa kwenda Hospitali pale wanapohisi wana vidonda kwenye miili yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya wenye ulemavu nchini Ernest Kimaya alisema,kama shirikisho la watu wenye ulemavu wameanza kukaa pamoja ili kutatua changamoto zinazowakabili katika maisha yao ya kila siku.

Kimaila,ameishukuru serikali  ambayo kuanzia mwaka 2012 imetoa ajira zaidi  214 kwa watu wenye ulemavu,hata hivyo ameiomba kuendelea kutoa kipaumbele kwa jamii ya watu wenye ulemavu.

Naye Mkurugenzi wa Kinga kutoka  Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Crispin Kahesa alisema, kati ya saratani zinazoongoza kwa watu wenye Ualbino ni saratani ya ngozi.

Alisema,kwa muda wa siku tatu wamefanikiwa kufanya uchunguzi kwa watu 370 ambapo kati ya hao watu 4 wameonekana na viashiria vya saratani na kutakiwa kwenda Hospitali ya Ocean Road kwa  uchunguzi zaidi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.