• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ASILIMIA 98 watoto Mbinga wana lishe bora

Imewekwa kuanzia tarehe: April 8th, 2021

Wananchi wa Wilaya ya Mbinga wametakiwa kuzingatia ulaji unaofaa na unaojumuisha makundi matano muhimu ya vyakula na matumizi ya mbolea za asili ikiwa ni jitihada za kutokomeza tatizo la udumavu na utapiamlo mkali Wilayani humo.

Hayo yamebainishwa leo Machi 31 wakati wa kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kilicholenga kujadili hali ya lishe ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kipindi cha kuanzia Oktoba hadi Machi 2020/2021 kilichofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Kiamili na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali ngazi ya Wilaya, Kata, mashirika yasiyo ya kiresikali, viongozi wa dini na wadau wengine wa lishe.

Katika kikao hicho cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kilichoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mhe. Cosmas Nshenye imeelezwa kuwa takribani 2% ya watoto waliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wana udumavu na utapiamlo mkali huku 98% ya watoto wakiwa na hali nzuri ya lishe, ushauri ukitolewa juu ya ulaji wa vyakula unaozingatia makundi matano ambayo ni wanga, protini, mbogamboga, mafuta na sukari hasa ya asili, na matunda mchanganyiko sambamba na udhibiti wa matumizi ya mbolea za viwandani ikiwa ni hatua muhimu na madhubuti katika mapambano dhidi ya udumavu na utapiamlo mkali Wilayani humo.

Akizungumza wakati wa Tathmini hiyo Mhe. Nshenye ametoa wito kwa viongozi wote wa ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji, wadau mbalimbali na wananchi kushirikiana kwa pamoja ili kuwa na jamii yenye uwezo wa kutoa maamuzi juu ya suala la lishe na kwamba kwa sasa ni vema jamii ikaelimishwa juu ya matumizi ya mbolea za asili (mboji na samadi) na kushirikishwa kwa ukaribu zaidi kwa maafisa ugani na idara ya kilimo katika jitihada za kupunguza matumizi ya mbolea za viwandani, lakini pia kuongeza matumizi ya chokaa kama ilivyopendekezwa na tafiti mbalimbali za hali ya udongo zilizofanyika Wilayani Mbinga.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Bw. Juma Mnwele amesema ataendelea kusimamia uwajibikaji wa kila mmoja na kwamba hatosita kuwachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kuwabadilisha vituo vya kazi wale wote watakaoonekana kusuasua katika mapambano dhidi ya utapiamlo na udumavu na kuboresha hali ya lishe kwenye maeneo yao suala ambalo pia linatekelezwa kitaifa kote nchini.

Kwa upande wao wajumbe waliohudhuria kikao hicho wamesema wao kama wadau muhimu tathmini hiyo imewapata fursa ya kujipima na kuona walipotoka, walipo na wapi wanaelekea katika mkakati wa kutokomeza hali ya udumavu na utapiamlo nchini na kuahidi kushirikiana kwa pamoja kufanyia kazi mapungufu na changamoto zote zilizobainishwa wakati wa kikao hicho.

Kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kimefanyika hufanyika kila robo kufuatia kusainiwa kwa mkataba huo kuanzia ngazi ya Taifa, Mkoa, Wilaya, Halmashauri, Kata na Vijiji lengo likiwa kufanya suala la lishe kuwa mtambuka sio la Idara na Wizara ya Afya pekee na kwamba ushiriano wa pamoja unahitajika ili kutoa huduma za lishe kwa jamii.

Imeandikwa na Salum Saidi

Afisa Habari Halmashauri ya Mbinga

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.