• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ASKARI WANYAMAPORI 150 wafuzu mafunzo Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: March 19th, 2024

Wizara ya Maliasili na Utalii inamatarajio makubwa ya kuimarika kwa shughuli za doria za kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu na hivyo kupunguza migongano baina ya binadamu na wanyamapori baada ya wahitimu zaidi ya kuhitimu fanyi ya uwaskari wa Wanyamapori.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Kamisha wa Polisi (CP) Benedict Wakulyamba alipokuwa akifunga mafunzo maalum kwa Askari Wahifadhi toka TAWA na kozi Na. 73/2024 kwa Askari Wanyamapori wa Vijiji (VGS) katika Chuo cha Likuyu Sekamaganga Wilaya ya Namtumbo Mkoa wa Ruvuma.

CP Wakulyamba ametaja matarajio mengine ya Wizara kwa wahitimu hao ni Pamoja na kuongezeka kwa ufanisi wa kuitikia kwa haraka kwenye matukio kutokana na kuwa, VGS mnaohitimu mtakuwa kwenye maeneo yenye changamoto na hivyo kuwa mstari wa mbele katika kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu kabla hawajasababisha Mathara.

Aidha CP. Wakulyamba ametoa wito kwa wananchi kuzingatia maelekezo yanayaotolewa na wataalamu wa taasisi za uhifadhi ili kuepuka madhara ya wanyamapori wakali na waharibifu, kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi katika maeneo yaliyopo jirani na hifadhi, mapito na mtawanyiko wa wanyamapori na kujiepusha na tabia ya kupiga wanyamapori wakali kwa kutumia silaha mbalimbali za kimila/jadi pindi wanapoingia kwenye maeneo ya wananchini.

Akimkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa cha Uhifadhi wa Vijiji kwa Jamii Likuyu Sekamaganga, Bi Jane Nyau ameeleza jumla ya Askari Wahifadhi ishirini na nane (28) toka kwenye Mapori ya Akiba ya Selous na Liparamba na VGS mia moja ishirini na mbili (122) kutoka Wilaya thelathini na nne (34) wamehudhuria mafunzo haya.

Naye Mkurugenzi wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo Dkt. Edward Kohi amesema Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia vyuo vyake vya mafunzo itaendelea kutoa Mafunzo mbalimbali ya Uhifadhi kwa kuwajengea uwezo Askari wa Jeshi la Uhifadhi pamoja na Askari wa Wanyamapori wa Vijiji ili kuimarisha Shughuli za Uhifadhi kwa kushirikiana na wanavijiji waishio jirani na Hifadhi.

Msimamizi Mkuu wa Mradi wa Frankfurt Zoological Society Bi. Kathryn Doody licha ya kuipongeza Serikali kwa kuendesha Mafunzo kwa askari wa Jeshi la Uhifadhi na VGS, amewakumbusha askari hao kutambua kuwa kazi wanayofanya ni muhimu sana, siyo kwa Tanzania tu bali kwa ulimwengu wote.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.