• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BILIONI 1.398 kufanyia matengenezo barabara za Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: February 21st, 2020

ASILIMIA  75 ya hali ya barabara katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma zina hali nzuri.

Kaimu Meneja wa TARURA katika Manispaa ya Songea Mhandisi  Henry Mtawa amesema barabara za Manispaa ya Songea zina jumla ya kilometa 390.88 ambazo ni sawa na asilimia 17.1  ambazo zina hali ya kuridhisha na kwamba kilometa 40.62  ambazo ni sawa na asilimia 7.8 zina hali mbaya.

Mhandisi Mtawa akitoa taarifa ya TARURA kwenye  Baraza la madiwani la Manispaa ya Songea, amesema katika mwaka  wa fedha wa 2019/2020 Halmashauri ya Manispaa hiyo imetengewa zaidi ya bilioni 1.398 ili kufanyia matengenezo mtandao wake  wa barabara.

“Matengenezo ya kawaida,zimetengwa zaidi ya shilingi milioni  342 ambazo zitatengeneza barabara za jumla ya kilometa kilometa 152.46’’,alisema.

Kulingana na Mhandisi huyo,fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara korofi  zenye urefu wa kilometa 28.13 ni zaidi ya milioni 181 na kwamba matengenezo ya muda maalum zimetengwa zaidi ya milioni 670.

Amezitaja fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya madaraja ni milioni 95 ambazo zitatumika kujenga madaraja madogo mawili na kufanyia matengenezo daraja moja na kwamba Manipaa ya Songea katika kipindi cha mwaka 2019/2020 imetenga shilingi milioni 324 za fedha za maendeleo kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Tunduru-Seedfarm yenye urefu wa kilometa 0.75 kwa kiwango cha lami nyepesi.

Hata hivyo amezitaja changamoto za barabara za vijijni na mijini katika Manispaa ya Songea kuwa ni  ufinyu wa bajeti ya matengenezo ya barabara ambapo ili kukabiliana na changamoto hiyo inatakiwa kuongeza bajeti ya matengenezo ili kuendana na uhalisia wa mahitaji ya matengenezo.

Wakizungumza baada ya kupokea taarifa baadhi ya  madiwani wametoa rai kwa TARURA kushughulikia haraka kero ya barabara katika Manispaa hiyo ambazo zimeharibika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hali ambayo imekuwa kero kubwa kwa wananchi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 21,2020.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.