• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ZAIDI ya bilioni tatu zilizotolewa na Rais Magufuli,zilivyoinufaisha Halmashauri ya Mji wa Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: May 28th, 2020

SERIKALI ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt John Magufuli imetoa zaidi ya shilingi biilioni tatu kwa Halmashauri ya Mji wa Mbinga mkoani Ruvuma kwa ajili ya ujenzi wa majengo tisa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga Grace Quentin ametoa taarifa ya miradi hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme alipokagua miradi hiyo ikiwemo nyumba ya Mkurugenzi iliyogharimu sh.milioni 300,nyumba saba za wakuu wa Idara zimegharimu sh.milioni 350 na jengo la Halmashauri limegharimu sh.bilioni 2.9 ambalo limekamilika na kuanza kutumika.

Akizungumzia mradi wa nyumba za watumishi na nyumba ya Mkurugenzi ambayo itakuwa na ghorofa moja,Quentin amesema mradi  kwa ujumla wake umefikia asilimia 70 na kwamba mradi ulianza kutekelezwa Aprili na unatarajia kukamilika Juni 2020.

“Mradi huu wa nyumba za watumishi utasaidia sana wakuu wa Idara,badala ya Halmashauri kuwalipa pango la nyumba,tutakuwa tumewasaidia nyumba hizi,mradi unafanyika kwa force account na  Msimamizi Mkuu wa mradi ni TARURA’’,anasema Quentin.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme kwa niaba ya wananchi wa Mbinga,amemshukuru Rais Dkt John Magufuli kwa kuruhusu kiasi hicho cha mabilioni ya fedha yaliyowezesha kujengwa jengo bora la Halmashauri ya Mji wa Mbinga.

“Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wetu kwa zawadi hii kubwa,kwa niaba ya serikali nawapongeza  wana Mbinga Mji kwa kupata jengo hili zuri na rafiki la kutolea huduma’’,alisisitiza.

Amesema kiasi hicho cha fedha kimejenga majengo tisa,moja la Halmashauri likiwa limekamilika na majengo mengine nane yakifikia asilimia 70 ya ujenzi ambapo amesisitiza kuwa kazi ni nzuri  ambapo ameahidi kuzipeleka Halmashauri nyingine kwenda kujifunza katika Halmashauri hiyo.

Hata hivyo amesema katika Mkoa wa Ruvuma anasimamia ujenzi wa majengo matatu ya Halmashauri yakiwemo Halmashauri ya Nyasa,Madaba na jengo la Mbinga Mji ambalo licha ya ujenzi wake kuanza nyuma limekamilika kabla ya waliotangulia kuanza ujenzi.

Amesisitiza kuwa Halmashauri ya Mji wa Mbinga wamekuwa mfano katika Mkoa kwa kukamilisha kazi na kuzishinda Halmashauri nyingine zilizopata fedha mapema na kuanza kazi mapema ambapo hadi sasa ujenzi wao haujakamilika hadi ameamua kuwapelekwa TAKUKURU kuchunguza.

Amemwagiza Mkurugenzi kuhakikisha kuwa jengo nzuri liwahudumia wananchi vizuri na kutoa maamuzi mema kwa manufaa ya wananchi wa Mji wa Mbinga na Tanzania.

IMEANDIKWA NA ALBANO MIDELO

AFISA HABARI WA MKOA WA RUVUMA

MEI 27,2020

MBINGA

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.