• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

CHAMA cha Ushirika cha Msingi Kimuli Mbinga chatoa milioni 100 kuchangia miradi ya maendeleo

Imewekwa kuanzia tarehe: July 13th, 2020

CHAMA cha Ushirika cha msingi kimuli,kilichopo kijiji cha Utiri, kata ya Utiri Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma, kimetoa sh. milioni 100, kwa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata ya Kitanda, Utiri na Kihangi mahuka.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Chama hicho Ernest Komba, wakati akisoma Taarifa ya utendaji kazi wa Chama hicho, Katika Ziara ya kukagua Shughuli za Chama hicho cha Msingi iliyofanywa na Viongozi wa Chama kikuu cha Ushirika Mbinga (MBIFACU) na viongozi wa ushirika ngazi ya Mkoa wa Ruvuma.

Komba amesema kuwa fedha hizo zilizotolewa na Chama cha kimuli, zilitokana na mapato ya premium na ziada, za Ndani na kusaidia ukarabati wa majengo ya Taasisi za elimu na Afya, zilizomo katika maeneo yanayohudumiwa na Chama cha kimuli.

Ameitaja miradi iliyopewa  fedha na chama hicho kuwa ni Zahanati ya Lipumba sh. milioni 14 ,Zahanati ya Kitanda milioni 9.5,  Zahanati ya Utiri  milioni saba na Sekondari ya  Ndela milioni 15.

 Miradi mingine ni Sekondari ya Kihangi Mahuka milioni 13,   Sekondari ya Luli milioni 2.5, Sekondari ya Ngwilizi milioni 1 ,na Shule za Msingi 10 zilizoko katika Kata ya Utiri na Kitanda, ambazo zimepewa milioni 26.

Amesema awali wananchi walikuwa wakichangia fedha za mifukoni, au kusubiri miradi itekelezwe na Serikali. Lakini kwa sasa Chama kimeona ni vema kufanya maendeleo hayo ili kurudisha fadhila kwa wananchi ambao huuza mazao  katika chama cha msingi ambapo hivi sasa wananchi wanaona faida ya uwepo wa chama cha Ushirika cha Msingi Kimuli.

“Chama kimetoa faida yake kwa kuchangia utekelezaji wa  miradi mbalimbali, ya Afya na elimu kwa kuchangia ukarabati na ujenzi wa madarasa kutokana na uhitaji wa taasisi husika, ili kuamsha ari kwa jamii na watambue umuhimu wa chama chao cha Ushirika, kwa kuwa kama sio chama kutoa kiasi hicho basi wangelazimika kuchangia au kusubiri  Serikali itoe fedha za kutekeleza miradi hiyo ya Maendeleo”, Alisema Komba.

Komba ametoa rai kwa Wananchi wa kata zilizo katika mradi,  huo wajiunge na Chama cha ushirika na Msingi Kimuli kwa Maendeleo ya kaya na Jamii kwa ujumla.

Licha ya kuchangia miradi ya maendeleo,Meneja huyo amezitaja, huduma zingine zinazotolewa kuwa ni mradi wa Mashine ya kusaga nafaka ambao hutoa huduma kwa wanachama, lengo likiwa ni kupata uzoefu na kupata uzoefu wa kuanzisha kiwanda cha kuchakata unga wa mahindi ambapo hivi  sasa chama kina mashine tatu katika Vijiji vya Utiri Mtama na Kitanda.

Kulingana na Meneja huyo Chama cha Ushirika cha Kimuli kimeanzisha  Mradi wa Mashamba ya miti ambapo mpaka sasa tayari wameshapanda ekari 30 za miti katika kijiji cha Kitanda, mahande na Mtama lengo likiwa ni kuwa ni kitega uchumi kitakachoongeza mapato katika chama hicho hapo baadaye.

Ili kuhakikisha wakulima wa kahawa wanaongeza uzalishaji wa zao la kahawa Komba amesema Chama kimekuza miche bora ya kahawa(Compact) ili kukuza hali ya uzalishaji wa zao hilo ambapo Katika Msimu huu Chama kimepanda miche ya kahawa 120,000.

Amesema miche hiyo imeoteshwa kitaluni na kuwauzia wakulima kwa bei rahisi ili wakulima waweze kuzalisha Kahawa bora.Pia chama kina mradi wa usafirishaji mizigo kwa kutumia magari ya Chama kwa lengo la kusafirisha mbolea,kahawa na vifaa vya ujenzi, ili kuongeza pato la Chama.

Kwa mujibu wa Komba,Chama hicho cha ushirika pia hukusanya Mazao ya wanachama na ya wakulima wengine kuyachakata na kuyatafutia soko la ndani na nje ya nchi ili kjuimarisha ushirika.

Kaimu Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya za Mbinga na Nyasa(MBIFACU) Henerck Ndimbo amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli kwa kuviongezea nguvu vyama vya Ushirika na Msingi kwa kuwa kwa sasa wakulima wengi mara baada ya kupata Elimu ya Ushirika wanauza mazao yao kupitia vyama vya ushirika na kupata manufaa mengi ikiwemo kusomesha watoto kununua pembejeo na kukuza pato la familia.

Kwa upande wake Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Ruvuma Bumi Masuba amekipongeza MBIFACU kwa kusimamia vema Vyama vya Msingi hali ambayo imewezesha kuimarisha ushirika kuanzia vyama vya msingi ambapo ametoa rai kwa wananchi kuvitumia Vyama vya Ushirika  vya Msingi vilivyoko katika Maeneo yao.

Mkoa wa Ruvuma wenye wilaya tano na Halmashauri nane  una jumla ya vyama vya ushirika 296 kati ya hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuna vyama 31,Hamashauri ya Mbinga 81,Namtumbo 59,Nyasa 15,Manispaa ya Songea 24,Tunduru 48,Halmashauri ya Madaba 8 na Halmashauri  ya Mji Mbinga 27.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 12,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.