• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC NAMTUMBO aipongeza MVIWATA kwa kutatua changamoto za wakulima

Imewekwa kuanzia tarehe: September 12th, 2021

MKUU wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Dr.Julius Ningu,ameupongeza mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania(MVIWATA)mkoani humo kutokana na kufanya ufuatiliaji katika sekta ya kilimo na kubaini changamoto ya baadhi ya miradi ya skimu za umwagiliaji kujengwa chini ya kiwango na mingine kushindwa kukamilika kwa wakati na kutoa tija kwa wakulima wa maeneo hayo.

Ningu alitoa pongezi hizo hivi karibuni katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa wilaya ya Namtumbo mara baada ya kupokea taarifa ya mrejesho wa ufuatiliaji wa raslimali za umma kupitia mradi wa utawala Bora unaotekelezwa na mtandao huo katika kata ya Ligera,Limamu na Kitanda wilayani humo kutoka kwa mratibu wa Mviwata wa mkoa wa Ruvuma Laika Haji.

Alisema kuwa Mviwata ni mdau mkubwa wa maendeleo katika kuisaidia serikali kwenye kutoa elimu kwa wakulima hivyo ameushauri mtandao huo kuendelea kupanua wigo wa utendaji wao wa kazi hususani katika kufanya tathmini wakati wa mavuno ya wakulima na kuzingatia takwimu pindi wanapofanya ufuatiliaji wa miradi mbalimbali badala ya kutoa elimu peke yake.

Kufuatia hali hiyo mkuu huyo wa wilaya ya Namtumbo Ningu amewaagiza wataalam wa idara ya kilimo wilayani humo kuzungukia miradi hiyo ya skimu za umwagiliaji zenye changamoto hizo ambazo ni za Namahoka Mwangaza na Mtakuja zilizopo katika kata hizo.

Aidha amewataka madiwani na wataalam wilayani humo kuhakikisha wanasimamia kikamilifu miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye kata zao kupitia ufadhili kwa lengo la kuwafanya wahisani waendelee kusaidia miradi hiyo ili iweze kuleta manufaa kwa wananchi na kwamba ameuomba mtandao huo kuangalia uwezekano wa kushawishi wadau mbalimbali wa kilimo kusaidia miradi hiyo ili iweze kukamilika.

“Mara nyingi miradi mingi ya kilimo cha umwagiliaji inashindwa kukamilika kwa wakati na kutoa tija kwa wakulima kutokana na ukosefu wa raslimali fedha na uchelewaji wa mapokezi wa fedha hizo za kuendeshea miradi hiyo”Alisema Ningu

Awali akizungumza katika kikao hicho ambacho kilishirikisha baadhi ya madiwani,wataalam pamoja na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo, mratibu wa Mviwata wa mkoa wa Ruvuma Laika Haji alisema kuwa mtandao huo tangu uanze kutoa elimu kwa wakulima na kufanya ufuatiliaji wa raslimali za umma katika sekta ya kilimo kupitia mradi wa utawala Bora umejaribu kuchochea kasi ya maendeleo kwa wakulima.

Naye katibu tawala wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Aden Nchimbi,akizungumza katika kikao hicho alisema kuwa wilaya hiyo imejipanga katika kuhakikisha inaboresha baadhi ya miradi ya kilimo cha umwagiliaji ili iweze kuleta tija na kuwainua wakulima kiuchumi.

Mkurugenzi mtendaji wa Halashauri hiyo Chiliku Chilumba akiongea kwenye kikao hicho alisema kuwa amepokea maagizo yote yaliyotolewa na mkuu wa wilaya ya Namtumbo Dr.Julius Ning una kuyafanyia kazi ikiwa pamoja na kuunda timu ya wataalam watakaozungukia miradi hiyo ya skimu za umwagiliaji kwa lengo la kuangalia changamoto mbalimbali.

Kwa upande wake mwezeshaji katika kikao hicho Mnung’a Shaibu Mnung’a alisema kuwa tangu Mviwata ianze shughuli ya ufuatiliaji wa miradi hiyo imeweza kubaini changamoto mbalimbali ikiwemo ya ukosefu wa uwazi na ushirikishwaji wa wananchi pindi miradi ya maendeleo inapotekelezwa kwenye maeneo yao.

Mnung’a ameishauri Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo kuacha tabia ya kuanzisha miradi mipya ya maendeleo kila mwaka na kuacha kukamilisha miradi viporo ambayo imeshindwa kukamilika kwa muda mrefu na kutoa tija kwa wananchi.

Imeandikwa na Julius Konala

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.