• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC Tunduru awaonya maafisa ugani matumizi ya pikipiki za serikali

Imewekwa kuanzia tarehe: June 25th, 2022

MKUU wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Julius Mtatiro,amekabidhi pikipiki 62 kwa maafisa ugani na  pikipiki 2 kwa maafisa ushirika wa Halmashauri ya Tunduru kwa lengo la kuwarahisishia kazi ya kuwafikia na kuwahudumia wakulima katika maeneo yao.


Akizungumza na wataalam hao alisema,pikipiki hizo zimetolewa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, kama mpango wake wa kuboresha sekta ya kilimo ili iweze kuleta tija kwa wakulima na Taifa.

Alisema,wakulima wa wilaya hiyo kwa muda mrefu  wameshindwa kufikia malengo ya uzalishaji kwa kuwa wanaendelea na kilimo cha mazoea kutokana na kukosa wataalam wa kuwapa elimu,hivyo matumaini yake kuwa pikipiki hizo zitakwenda kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi kupitia sekta ya kilimo.

“ndugu zangu maafisa ugani,serikali imetoa malengo ya kuzalisha tani laki nne za korosho nchi nzima, na sisi wilaya yetu imepewa lengo la kuzalisha tani elfu thelathini na tano katika msimu wa kilimo 2022/2023,hivyo kupitia kwenu lazima tufikie malengo hayo”alisema.

Mkuu huyo wa wilaya,ameagiza pikipiki hizo ziwasaidie maafisa ugani kuwatembelea wakulima kwa wakati kwa ajili ya kuwapa  huduma za ugani ili waachane na kilimo cha mazoea.

Mtatiro alisema,  uzalishaji ukioongezeka upo uwezekano mkubwa pia mapato ya Serikali kupitia Halmashauri ya wilaya yataongezeka, ambapo ametoa siku kumi na nne kwa vongozi wa Halmashauri hiyo kupeleka mpango kazi ofisini kwake  namna maafisa ugani hao watakavyoweza kumudu gharama za uendeshaji wa pikipiki hizo.

Amewakumbusha maafisa ugani kwamba, wana wajibu wa kuhakikisha pikipiki walizopewa  zinatumika kwa shughuli iliyokusudiwa ikiwani pamoja na kuwahudumia wakulima  kwani itasaidia wakulima kutokuwa na manung’uniko ya kutofikiwa na wataalam hao.

Amewaomba kutomwangusha Rais Samia Hassan kutokana na kazi kubwa ya kusaidia na kuinua sekta ya kilimo hapa nchini,kwa hiyo ni mategemeo ya serikali kuwa, pikipiki hizo zitatumia kuleta mapinduzi makubwa ya kilimo katika wilaya hiyo.

Hata hivyo alisisitiza kuwa,afisa ugani yeyote atakayebainika kugeuza matumizi ya pikipiki hizo kuwa bodaboda atanyang’anywa ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

Mtatiro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo, amewaasa maafisa ugani hao kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali  zisizo za lazima na kuepuka kuwabeba watu wasiowafahamu wanaoweza kuwateka na kuwapora pikipiki.

“mjihadhari sana kuwabeba watu wa onyo ovyo,kuna wengine sio waaminifu watawanyonga na kuwapokonya pikipiki hizi”alisema Mtatiro.



Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya Tunduru Jonathan Haule, amewataka kuzingatia na kufuata sheria za barabarani na kuwa na matumizi sahihi  ya kwenda kuwasaidia wakulima walime kilimo chenye tija.


Akizungumza kwa niaba ya wenzake  Afisa kilimo wa kata  ya Tinginya Jamal Said,amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia usafiri huo kwani kwa muda mrefu wamekuwa wakipata shida kuwatembelea wakulima.


Jamal alisema, pikipiki hizo walizopewa na Serikali watakwenda kufanya mapinduzi makubwa ya kilimo na kuongeza uzalishaji wa mazao  kwa wakulima wa wilaya hiyo ya Tunduru.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.