• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI mbili Songea zapata hati safi

Imewekwa kuanzia tarehe: June 25th, 2022


Halmashauri  za Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Songea mkoani Ruvuma zimepata hati safi kutokana na ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) uliofanyika kuishia Juni 30 mwaka huu.

Akizungumza kwa nyakati tofauti kwenye vikao maalum vya kujadili taarifa ya CAG katika  mabaraza ya madiwani katika Halmashauri hizo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amezipongeza Halmashauri hizo kwa kufanikiwa kupata hati safi.

Akizungumza katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Ibuge ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kuweza kukusanya mapato ya ndani kwa asilimia 94.67 ya lengo la kukusanya mapato Zaidi ya shilingi bilioni 3.97 ambapo wameweza kukusanya Zaidi ya shilingi bilioni 3.76 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021.

“Nitumie nafasi hii kuelezea masikitiko yangu kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuchangia asilimia 43.06 tu kwenye mfuko wa wanawake,vijana na watu wenye ulemavu ambapo mmeweza kuchangia shilingi 138,100,00 tu kati ya shilingi 320,715,281 ambazo mlipaswa kuchangia’’,alisisitiza Ibuge.

Akizungumza katika  kikao maalum cha CAG katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea,Mkuu wa Mkoa ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kukusanya mapato ya ndani kwa asilimia 79 katika mwaka wa fedha unaoishia Juni 30 mwaka huu.

Amesema katika kipindi hicho Halmashauri hiyo iliweza kukusanya kiasi cha Zaidi ya shilingi bilioni 1.32 kati ya lengo la kukusanya Zaidi ya shilingi bilioni 1.67 katika mwaka wa fedha 2020/2021.

Hata hivyo amesisitiza kuwa makusanyo hayo bado ni  chini ukilinganisha na kiwango kilichowekwa cha kukusanya angalau asilimia 81 ya lengo.

RC Ibuge pia amesikitishwa na Halmashauri hiyo kuchangia asilimia 50.3 tu ya mfuko wa wanawake,vijana na wenye ulemavu ambapo wameweza kuchangia Zaidi ya shilingi milioni 66 tu kati ya Zaidi ya milioni 132 ambazo zilipaswa kuchangiwa katika kipindi hicho.

Katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa ameagiza Halmashauri zote kuhakikisha hoja zote zilizosalia zifungwe na kuzuia kujirudia kwa hoja na kwamba wakuu wa Idara washiriki kikamilifu kuandaa majibu ya hoja na utekelezaji wa mapendekezo ya CAG.

Mkuu wa Mkoa pia ameagiza Halmashauri zote  zichukue mapema hatua za kinidhamu kwa watumishi wanaozalisha hoja,pia ameagiza kudhibiti upotevu wa mapato katika Halmashauri na kwamba Halmashauri ziendelee kulipa madeni mbalimbali ya wazabuni kwa wakati ili kujiendesha kwa tija.

RC Ibuge pia ameziagiza Halmashauri kusimamia kikamilifu mfuko wa Bima ya Afya na Bima ya Afya iliyoboreshwa ili kila mwananchi aweze kujiunga ikiwa ni Pamoja na kufuatilia malipo yake kwenye vituo vya afya na zahanati.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Mheshimiwa Michael Mbano na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mheshimiwa Menace Komba wameahidi maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa kuyafanyia kazi kwa haraka.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 25,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.