• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Madaba inaardhi nzuri kwaajili ya Uwekezaji wa Kilimo cha Biashara na Chakula

Imewekwa kuanzia tarehe: November 24th, 2020

HALMASHAURI ya Wilaya ya Madaba inamaeneo mazuri ya Uwekezaji wa Viwanda pamoja na Uwekezaji wa kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula na Biashara.

Akitoa taarifa hiyo Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Shafi Kassim Mpenda amesema anawakaribisha wawekezaji katika Halmashauri ya Mdaba kwakuwa Ardhi ya Madaba inafaa kwa kilimo cha mazao ya Biashara,chakula na Viwanda.

‘’ kufikia Juni 2019 Halmashauri hiyo ilikuwa na wawekezaji wakubwa wa 4, Silverland Ndolela anafanya shughuli  za kilimo cha mazao na ufugaji eneo la Hekta 5,000,Wakala wa misitu Tanzania (TFS)anafanya shughuli za upandaji wa miti eneo la vijiji vya ifinga Wino na Mkongotema zaidi ya Hekta 24,000,Chuo kikuu cha Sokoine Hekta 10,000 kijiji cha Ifinga wamepanda miti zaidi 2,000,Mbangamawe partiners anazalisha chokaa katika kijiji cha Mtyangimbole”.

Aidha amesema Mwekezaji wa kampuni ya Ifinga food processing anaongeza thamani ya mazao kwa kufungasha kama Tangawizi,na Mwekezaji mwingine Kampuni ya Interfruit Limited ya Mjini Songea inatarajia kuwekeza kwenye kilimo cha matunda ya Parachichi Hekari 3,000 na kujenga Kiwanda cha kusindika matunda mara yatakapoanza kuvunwa katika kijiji cha Mahanje.

Vile vile Mkurugenzi amesema Halmashauri ya Wilaya ya Mdaba inazalisha mazao ya kilimo kama Miti ya Mbao,fito,nguzo za umeme/simu,kilimo cha Kahawa,Tangawizi,Matunda,Mpunga na Mazao ya Mafuta.

“Matarajio ya Halmashauri ni kupokea wawekezaji wakubwa kwenye sekta ya kilimo na umwagiliaji ili watumie maeneo mazuri yaliyopo kwenye eneo letu,Kuwapokea wawekezaji wa kujenga viwanda vya kuchakata  mazao ya misitu(Miti) na Nafaka Mahindi)”.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo akielezea maeneo yanayotambulika kwa kuwekeza  amesema Kitongoji cha Ifungwa kijiji cha Madaba kilo mita 10 kutoka Barabara kuu Songea- Njombe  kina Hekari 400 eneo hilo limetengwa kwaajili ya Uwekezaji wa Kiwanda  au shughuli yoyote kwa kuwekeza katika eneo hilo.

Amesema eneo la Itombolo lina Hekta 2000 lipo katika Kijiji cha Mkongotema mpakani na kijiji Lutukila kandokando ya Barabara kuu ya Songea-Njombe ni eneo lililotengwa kwaajili ya shughuri ya Viwanda vya kuchakata  mazao ya Mahindi,Tangawi na Mzao Mengine, eneo hilo ni mali ya Kijiji Halmashauri na Kijiji watahakikisha  Mwekezaji anapata Eneo analihitaji ili wananchi wanufaike na fursa na kazi zitakazoendelea eneo hilo.

Akiendelea kuelezea maeneo ya kuwekeza katika Halmashauri hiyo amesema kuna Hekta 4,200(Hekari) ni shamba la Mifugo  na ni Mali ya Wizara ya Mifugo  lipo kando ya Barabara kuu Songea-Njombe,Halmashauri ya Madaba inatunza na kulitumia amesema Wawekezaji wanakaribishwa kwaajili ya shughuri ya ufugaji  mifugo ya (Ng’ombe),kwa sasa kuna wafugaji waliokodishwa vitalu 16 na bado kuna nafasi  ya vitalu 8 na eneo limepitiwa na mto mkubwa unaowezesha kutumika kwa uzalishaji wa chakula cha Mifugo.

“Halmashauri ya Wilaya ya Mdaba inamiliki eneo lenye Hekari 500 lipo km 18 kutoka Barabara Kuu Songea Njombe ukielekea Kijiji cha Ifinga na eneo Hilo lipo tayari kwaajili ya  mwekezaji kuwekeza kwa shughuli za kilimo hasa kilimo cha Miti,Kahawa,na Mazao mengine yanayoendana pamoja na maporomoko ya Umeme Masigira,Lipupuma,na Lingatunda”.

Pia Halmashauri ya Madaba na vijiji vyake 21 inamaeneo ya kutosha hivyo yeyote anakaribishwa kuwekeza katika maeneo hayo na vijiji 11 vimepimwa Halamashauri itahakikisha mwekezaji anapata eneo la kutosha analohitaji katika kijiji chochote kwa kilimo cha mazao.

Halmashauri ya Madaba inatoa rai kwa wawekezaji kuwekeza katika Viwanda mbalimbali kwenye mji wa Madaba na Vijijini ikiwa tayari vijiji 19 vinaumeme wa uhakika,kutokana na malighafi zilizopo Viwanda vya uchakataji wa Mazao ya Misitu  na Usindikaji.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Halmashauri ya Madaba

Novemba 24,2020.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.