• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Mbinga yafanya ziara ya mafunzo Halmashauri ya Madaba

Imewekwa kuanzia tarehe: April 8th, 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Juma Mnwele ameongoza Timu ya Wataalamu wa Halmashauri hiyo na kufanya ziara ya kutembelea Halmashauri ya Wilaya ya Madaba kujionea namna miradi mbalimbali ya maendeleo inavyotekelezwa na Halmashauri hiyo.

Ziara hiyo ya Wataalamu kutoka Mbinga imefanyika leo Aprili 6, 2021 ambapo wamepata nafasi ya kutembelea miradi mikubwa mitatu ya Jengo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), Nyumba ya Mkurugenzi na Nyumba 6 za Wakuu wa Idara, miradi ambayo imetekelezwa na inayoendelea kutekelezwa na Halmashauri hiyo ya Wilaya ya Madaba kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza wakati wa kikao cha pamoja kati ya Wataalamu wa Halmashauri zote mbili za Mbinga na Madaba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Bw. Juma Mnwele amesema wanatambua na kuthamini namna Madaba wanavyotekeleza na kusimamia miradi yao hususani jinsi walivyokamilisha ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji na miradi mingine inayoendelea kutekelezwa na wao (Mbinga) wameona ni sehemu nzuri ya kujifunza kupitia wao.

Naye mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Bw. Shafi Mpenda amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na timu yake ya wataalamu kwa kutembelea Madaba na kuongeza kuwa wamefarikija sana na ujio wa timu hiyo na anaamini baada ya ziara hiyo Mbinga itafanya vizuri zaidi ya walivyofanya wao Madaba katika utekelezaji wa miradi yake ya ujenzi mathalani ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W).

Ziara hii ya Timu ya Wataalamu wa Halamshauri ya Wilaya ya Mbinga ni kufuatia Halmashauri hiyo kupokea fedha kiasi cha Tshs. Bilioni Moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, mradi utakaotekelezwa kwa kutumia Force Account, utaratibu unaohusisha Halmashauri kuwa na majukumu na wajibu wa kufanya ununuzi wa vifaa na usimamizi wa ujenzi kupitia kamati mbalimbali badala ya kutumia wakandarasi kama ambavyo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba imekamilisha ujenzi wa jengo lake kwa mafanikio makubwa.

 Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga inatarajia kuanza ujenzi wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji hivi karibuni katika eneo la Kiamili lililopo ndani ya Mji mdogo wa Kigonsera kwa kutumia Force Account, ujenzi ambao utahusisha usimamizi wa karibu wa wataalamu hao kupitia Kamati za Ujenzi, Ununuzi, Ukaguzi na Mapokezi ambapo kupitia ziara hiyo ya kutembelea Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, timu hiyo imepata chachu, morali na ari mpya ya kufanya vizuri ili kuleta ufanisi katika usimamizi wa miradi mbalimbali ndani ya Halmashauri hiyo.

Imeandikwa na Salum Said

Afisa Habari Halmashauri ya Mbinga

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.