• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Mji Mbinga yapata hati safi miaka mitatu mfululizo

Imewekwa kuanzia tarehe: May 28th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ameipongeza Halmashauri ya Mji wa Mbinga  kwa kuendelea kupata hati safi tangu kuanzishwa kwa Halmashauri hiyo miaka mitatu iliyopita.

Mndeme ametoa pongezi hizo wakati anafungua kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo cha kujadili taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)  kwa mwaka wa fedha za 2018/2019 mjini Mbinga.

Taarifa ya CAG  inayoishia Juni 30,2019 imeonesha kuwa Halmashauri ya Mji wa Mbinga imepata hati safi na kwamba mwenendo wa hati za ukaguzi katika Halmashauri hiyo imekuwa ni wa kuridhisha kwa miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka wa fedha wa 2016/2017 hadi 2018/2019.

“Napenda niwakumbushe kuwa kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo sio jambo dogo,hongereni sana,hivyo naomba niwape shime kwamba kupatikana kwa hati hizo kuwafanye muongeze bidii zaidi’’,alisisitiza.

Mndeme pia amewapongeza madiwani na watalaam wa Halmashauri hiyo kwa kuweza kuchangia kwa asilimia 100 mfuko wa wanawake,vijana na wenye ulemavu ambao wamechangia zaidi ya shilingi milioni 112.

Katika kikao hicho,Mndeme ametoa maagizo kwa uongozi wa Halmashauri hiyo ambayo ni kuzuia kuwepo kwa hoja zinazojirudia mwaka hadi mwaka,wakuu wa Idara kushiriki ipasavyo katika kuandaa majibu ya hoja,utekelezaji wa mapendekezo ya CAG  na kuchukua hatua kwa watumishi wanaozalisha hoja.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga Grace Quentin,akizungumza katika kikao hicho,amesema makusanyo ya mapato ya ndani katika mwaka wa fedha wa 2018/2019.makisio yalikuwa ni kukusanya zaidi ya bilioni 1.4 hata hivyo makusanyo halisi yalikuwa ni zaidi ya bilioni 1.5 sawa na asilimia 107.15.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga David Mapunda ameahidi kusimamia utekelezaji wa maagizo yote aliyoyatoa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ili kuhakikisha kuwa Halmashauri hiyo inaendelea kuwa mfano kwa Halmashauri nyingine.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas Nsenye ameyataja mafanikio yaliyopatikana katika wilaya hiyo ikiwemo kupata hati safi na kukamilisha miradi kwa wakati,yametokana na uwepo wa ushirikiano na mshikamano baina ya madiwani na watalaam.

Halmashauri ya Mji wa Mbinga ni miongoni mwa Halmashauri sita kati ya nane zilizopo katika Mkoa wa Ruvuma zilizopata hati ya safi kwenye ukaguzi wa  CAG  wa mwaka wa fedha 2018/2019.

IMEANDIKWA NA ALBANO MIDELO

AFISA HABARI WA MKOA WA RUVUMA

MEI 28,2020

MBINGA

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.