• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Songea yaingia mkataba kukusanya ushuru

Imewekwa kuanzia tarehe: March 15th, 2021

Halmashauri ya wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma imeingia mkataba na kampuni ya West Food Comp LTD ya kutoka Makambako Mkoani Njombe kwa ajili ya kukusanya ushuru wa mazao.

Makubaliano ya mkataba huo yamefanyika  katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kwa kuwekeana saini baina ya Mkurugenzi wa Kampuni na Uongozi wa Halmashauri.

Akisaini mkataba huo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Tanu Kameka ametoa wito kwa Kampuni hiyo kufanya kazi waliyoomba kwa ufanisi kwasababu Serikali inategemea mapato kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni hiyo Godwin Chengula ameahidi kufanyakazi kwa ufanisi  na kwamba ana uzoefu katika kazi ya ukusanyaji ushuru ambayo ameifanya katika maeneo ya Wilaya za Ulanga ,Ifakara ,Makambako na Manispaa ya Songea

Naye Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo Rajabu Lingoni amesema katika kuboresha ukusanyaji wa mapato vikao vya kisheria vilikubaliana kumpata mzabuni atakayefanya kazi ya ukusanyaji wa ushuru wa mazao badala ya kuendelea kuwatumia mawakala.

“Maamuzi hayo yamefikia baada ya kubaini udanganyifu mkubwa katika ukusanyaji wa ushuru,unaofanywa na baadhi watendaji wa Kata kupitia mawakala wao kitendo ambacho kilikuwa kinakwamisha jitihada za Halmashauri katika kutekeleza majukumu yake’’,alisisitiza.

Lingoni amesema jumla ya vizuio 15 vimeanishwa na vimekabidhiwa kwa mzabuni ambavyo vitatumika katika kukusanya ushuru wa mazao katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia  Machi 2021hadi Machi 2022.

Hata hivyo amesema mzabuni anatakiwa kukusanya ushuru kwa kuzingatia taratibu,kanuni na sheria za ukusanyaji wa mapato zilizowekwa na Serikali.

Kwa upande wake Mhasibu wa Mapato wa Halmashauri hiyo Noel Chengula  ameutaja utaratibu wa kutoa zabuni katika kazi ya ukusanyaji ushuru ni kitendo kitakachoongeza ufanisi na kuondoa usumbufu na gharama za kuwalipa mawakala ambao awali walikabidhiwa jukumu hilo.

Chengula amesema jambo hilo litapunguza changamoto ya madeni kwa baadhi ya Watendaji wa Kata,Vijiji na mawakala na kwamba gharama za ufuatiliaji,na fedha za makusanyo zitafikishwa benki kwa wakati.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 15,2021

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.