• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HATI yenye mashaka ilivyomsitikisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: June 6th, 2020

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma imepata hati yenye mashaka kwa ripoti  ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme akifungua kikao Maalum cha Baraza la madiwani la Halmashauri hiyo cha kujadili hoja na mapendekezo ya CAG kilichofanyika Ikulu ndogo ya Songea,amesema ameumizwa na kusitikishwa na hati hiyo ambayo ni ishara kuwa hakuna ushirikiano kati ya madiwani na wataalam.

“Nachukua fursa hii kwa namna ya pekee kutoa masikitiko yangu hati yenye mashaka imeniumiza na kunisikitisha sana’’,alisema Mndeme.

Kutokana na hati yenye mashaka Mndeme amewaagiza madiwani na watalaam wa Halmashauri ya Songea kuongeza nguvu katika utendaji kazi na kuimarisha mshikamano na umoja ili hali hiyo isijitokeza tena.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amesema,licha ya kupata hati yenye mashaka kwa mwaka 2018/2019,mwenendo wa hati za ukaguzi kwa miaka minne katika halmashauri hiyo unaonesha kuwa mwaka 2015/2016 Halmashauri ilipata hati yenye mashaka,2016/2017, hati inayoridhisha, 2017/2018 hati inayoridhisha na 2018/2019 hati yenye mashaka.

Amesema ndani ya miaka minne Halmashauri hiyo imepata hati mbili zenye mashaka,hali ambayo amesema ni ishara tosha ya kukosekana kwa uwajibikaji ambapo ameagiza kila mtumishi kutimiza wajibu wake pamoja na kusimamia matumiz sahihi ya fedha za umma.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa ametoa siku saba kwa  Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuwalipa madiwani posho zao zote wanazodai ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 36.

Mndeme pia ameagiza kufunguliwa ofisi na kuwepo mtaalam katika shamba la kahawa la  AVIV lililopo katika kijiji cha Lipokela ambalo ni chanzo kikubwa cha mapato ya ndani katika Halmashauri hiyo.

“Naagiza mtaalam huyo kukusanya takwimu za uzalishaji na mauzo ya kahawa katika shamba hilo ili serikali iweze kupata mapato sahihi,pia kupitia shamba hili,amashisheni wakulima  kulima kahawa’’,alisisitiza Mndeme.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Rajabu Mtiula amemuomba radhi Mkuu wa Mkoa  kutokana na Halmashauri hiyo kupata hati yenye mashaka ambapo amemthibitishia hali hiyo haitarudia tena na kwamba maagizo yote aliyotatoa watayafanyia kazi.

Halmashauri ya Wilaya ya Songea na Halmashauri ya Manispaa ya Songea ni miongoni mwa Halmashauri mbili kati ya nane zilizopo mkoani Ruvuma ambazo zimepata hati zenye mashaka katika ukaguzi wa CAG wa mwaka wa fedha 2018/2019.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 6,2020

Songea

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.