• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HAYATI SONGAMBELE aacha alama,kitabu chake kuwa rejea kuu ya Taifa

Imewekwa kuanzia tarehe: June 4th, 2025

Katika anga ya majonzi , taifa linamsindikiza mmoja wa wazee wake mashuhuri, Hayati Alhaj Mohamed Mustafa Songambele. 

Katika tukio hilo la kihistoria lililofanyika Mahenge mjini Songea mkoani Ruvuma, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amefichua urithi mkubwa alioacha Mzee Songambele,kitabu cha kihistoria kiitwacho “Safari ya Karne”, ambacho kimetajwa kuwa hazina ya kipekee katika kuelezea historia ya uhuru na maendeleo ya Tanzania.

Akitoa salamu za pole kwa niaba ya CCM na Serikali, Balozi Nchimbi alisema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameagiza shughuli zote za msiba huo kugharamiwa na Serikali, ikiwa ni heshima kwa mchango mkubwa wa Hayati Songambele katika ujenzi wa taifa. 

Alisisitiza kuwa CCM itasimamia mchakato wa uchapaji wa kitabu hicho ili kizazi cha sasa na kijacho kipate maarifa ya kina kuhusu harakati za ukombozi na msingi wa Tanzania ya leo.

Kitabu cha Safari ya Karne kinaelezea kwa kina maisha na mchango wa Mzee Songambele, kuanzia mapambano ya uhuru, uhusiano wake wa karibu na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, hadi kuundwa kwa Tanzania na hatimaye kuzaliwa kwa CCM. 

Balozi Nchimbi alieleza kuwa awali kitabu hicho kilipendekezwa kiitwe Swahiba wa Nyerere, lakini baadaye Mzee Songambele alikibadilisha jina baada ya kutambua kuwa anakaribia kutimiza miaka 100 ya maisha yenye historia nzito.

“Alinikabidhi niandike dibaji ya kitabu hicho na nilifanya hivyo kwa moyo wote,” alisema Balozi Nchimbi kwa hisia. 

Alimwelezea Hayati Songambele kama kiongozi mwenye maono, aliyetoa mchango usio na kifani katika siasa na maendeleo ya taifa, akiwa chimbuko lake ni Mkoa wa Ruvuma.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NMB yatoa madawati 150 ya milioni 16 Songea

    June 05, 2025
  • UCHANGIAJI damu wazidi kuimarika Ruvuma

    June 04, 2025
  • TRILIONI 1.18 za Rais Samia zavunja ukame wa maendeleo Ruvuma,ndani ya miaka minne Ruvuma yachanua

    June 04, 2025
  • RAS RUVUMA alivyowaongoza wananchi kuchangia damu

    June 04, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.