• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HUDUMA za meli katika ziwa Nyasa zinavyochochea uchumi wa Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: April 3rd, 2023

Pichani ni meli ya MV Mbeya II ikiwa imetia nanga katika bandari ya Mbambabay wilayani Nyasa

SERIKALI imenunua meli tatu zinazotoa huduma za abiria na mizigo katika mikoa ya Ruvuma,Mbeya na Njombe kupitia ziwa Nyasa.

 Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) inahudumia jumla ya bandari 15 katika ziwa Nyasa ambapo katika Mkoa wa Ruvuma,TPA inahudumia bandari sita ambazo  ni  Mbambabay,Liuli,Njambe,Lundu,Mkili na Ndumbi,katika Mkoa wa Njombe TPA pia inahudumia bandari sita ambazo ni  Lumbila, Ifungu, Nsisi, Makonde,Lupingu na Manda na  katika Mkoa wa Mbeya TPA inahudumia bandari tatu ambazo ni Itungi,Kiwira na Matema.

Baadhi ya bandari TPA imeweka miundombinu ya kisasa,pia kuna bandari ambazo zinaendelea kuwekwa miundombinu kwa ajili ya utoaji huduma bora na za kisasa.

Kila bandari inahitaji kuwa na magati,maghala,yadi za kutunzia mitambo na mizigo na uwepo wa nyumba za kuishi wafanyakazi,sanjari na kuweka mifumo ya  zimamoto,majisafi,maji taka na mifumo ya TEHAMA ili kufanyakazi kwa ufanisi na tija kulingana na maelekezo ya serikali.

Ili kuboresha huduma katika bandari zote za ziwa Nyasa,TPA inatekeleza mpango kabambe unaoanza mwaka 2021/2022 na unaotarajia kukamilika katika kipindi cha mwaka 2028/2029.

Mpango huo kabambe utaongeza shehena ya mizigo katika ziwa Nyasa kutoka tani zaidi ya 11,000 hadi kufikia shehena ya mizigo zaidi ya tani 100,000,lengo hili linachochewa na mipango mizuri ya serikali ikiwemo kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya lami toka Mbinga hadi Mbambabay.

kutokana na kukamilika kwa lami ya Mbinga hadi Mbambabay na kuanza kutoa huduma za meli katika ziwa Nyasa kunafufua uchumi wa mji wa Mbambabay wilaya ya Nyasa  hivyo kuunganisha Tanzania kupitia ushoroba wa Mtwara na nchi za Malawi,Msumbiji , Zimbabwe na Zambia.

Hakuna ubishi Mji wa Mbambabay utafufuka kwa kasi kutokana na kukamilika kwa mtandao wa barabara ya lami kutoka Mbinga hadi Mbambabay na serikali kununua meli tatu mpya  kati ya hizo meli mbili za MV Njombe na MV Ruvuma ni za mizigo na meli moja ya MV Mbeya II ni ya abiria.

Kulingana na TPA meli zote tatu zimegharimu zaidi ya shilingi bilioni 20.1  ambazo zimetolewa na serikali kujenga meli kwa kutumia  kampuni ya Songoro Marine inayomilikiwa na Mtanzania.

Meli mbili za mizigo MV Njombe na MV Ruvuma kila moja ina uwezo wa kubeba tani 1000 na kwamba kila meli imegharimu shilingi bilioni 5.5 na meli ya abiria ya MV Mbeya II ina uwezo wa kubeba abiria 300 na mizigo tani 200, imegharimu shilingi bilioni 9.1.

Kwa mujibu wa taarifa ya TPA meli ya abiria ya MV Mbeya II  imerithi jina la meli ya MV Mbeya I iliyozama eneo la Makonde ziwa Nyasa mwaka 1977.

Hata hivyo  meli ya MV Mbeya II baada ya kujengwa iliingizwa majini Septemba 2019

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas anasema  wilaya ya Nyasa sasa imefunguka kutokana na kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya lami toka Mbinga hadi Mbambabay na kuanza rasmi kwa huduma za meli tatu ndani ya ziwa Nyasa.

Amesema huduma za meli zinaimarishaji bandari katika ziwa Nyasa na kuchochea shughuli za kiuchumi hususani biashara na uwekezaji  na sekta ya utalii.

Mkuu wa Mkoa  anatoa rai kwa watanzania waliopo ndani na nje ya nchi kufika kuwekeza katika wilaya ya Nyasa  ambayo miundombinu yake imeboreshwa ikiwemo barabara ya lami,umeme na usafiri wa majini.

Mhandisi Stella Manyanya ni Mbunge wa Jimbo la Nyasa anasema kuboreshwa kwa barabara na uwepo wa meli mpya kutaongeza idadi ya wageni wanaotembelea wilaya Nyasa ambayo ni kitovu cha utalii katika Mkoa wa Ruvuma.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Aprili 3,2023

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.